image slider

HUDUMA TUNAZOZITOA
Watengenezaji wa mashine za kuangulia vifaranga vya kuku
Wauzaji wa vifaranga vya kuku
Ushauri wa ufugaji wa kuku
Mashine za kuangulia vifaranga vya kuku
Wauzaji wa vifaranga vya kuku
Mashine za kuangulia vifaranga vya kuku

Sunday, December 19, 2010

CCM WATANGULIZE MASLAHI YA WANANCHI

  Kuna mambo mengi sana yanayowachefua Watanzania sasa. Harakati zilizoendeshwa ili kutusaidia kupata uhuru zililenga kumkomboa Mtanganyika kuondokana na umaskini, ujinga na maradhi.
   Leo hii baada ya miaka 49, Watanzania wamekuwa na hali mbaya nafikiri kuliko hata hali waliyokuwa nayo miaka ya sabini. Sisi Watanzania tukae tufikiri kwa makini ili tujue kosa letu liko wapi.
   Kama kweli tunataka kuondokana na shida tulizonazo tusiogope kuambiana ukweli pale mmoja wetu anapotusaliti na kusababisha turudi nyuma kimaendeleo.
   Kwanza kabisa tunasikia miaka hiyo kulikuwa na chama kilichoitwa TANU na baadaye jina likawa CCM. Chama hiki kimekuwa madarakani toka tunapata uhuru. Kama chama hiki kimekuwepo madarakani muda huo wote, na serikali yake ndio ilikuwa na wajibu wa kuondoa matatizo Tanzania na hayo matatizo hayajaondoka lawama ziende kwa nani. Kwa uelewa wangu CCM wabebe lawama ya kutufanya Watanzania tubaki na hali mbaya mpaka leo.
   SERIKALI ya CCM inakiri kwamba Tanzania bado tu maskini sana. Hii ilionekana pale mwenyekiti wao aliposema hawezi kuongeza kima cha chini cha mshahara kufikia Tsh.350000.
   Hivi jamani Watanzania, nani hajui maisha ya leo hapa Tanzania mtu hawezi kuishi kwa dola mbili. Sasa fikiri serikali inalazimisha watu wake waishi kwa dola mbili wakati haiwezekani. Je, hapo utategemea umkute mtu au mfanyakazi ana afya inayomwezesha kufanya kazi kwa furaha? Jibu la kweli ni hapana. Mtu akiwa ofisini ataendelea kufikiri namna ya kupata chochote kwa njia nyingine ili aweze kutimiza mahitaji kule nyumbani.
   SERIKALI imeshindwa kusimamia raslimali za taifa letu ili wananchi wake wafaidike nazo. Hakuna mtu anayebisha hilo. Hebu tuone fedha zinazotumika kuzalisha umeme. IPTL, RICHMOND na mengine mengi yametuchukulia fedha nyingi ajabu. Toka miaka hiyo yote ya uhuru tumeshindwa nini kuhakikisha sisi wenyewe tunaazisha miradi mikubwa ya kuzalisha umeme unaotutosha badala ya kukodi makampuni hewa kama RICHMOND. Hiki ni kielelezo kwamba serikali ya CCM imeshindwa kufanya kazi.
   Mifano mingine midogo kabisa ni kama pale serikali iliposhindwa kutuambia wananchi kampuni za kagoda ni za nani maana nazo zilichukua mabilioni ya walipa kodi. Bado hatujakaa sawa tunaambiwa tunatakiwa kuilipa DOWANS Tsh. bilioni 185. Hivi jamani hawa watawala wetu wametupeleka wapi mpaka tunaingia hasara hizi. Tumefanya uchaguzi jana tu. Wananchi wamechagua viongozi wao. Kwa kuwa kumekuwa na usiri na kutoaminiana kwa mazingira ya uchaguzi kugubikwa na mazingira ya wizi leo hii kesi za kupinga matokeo sehemu mbalimbali zimefunguliwa. Kwa hilo tu tayari tunatakiwa kutoa Tsh. zaidi ya bilioni mbili.
  Mnafikiri kwa hayo yote yanayoendelea kuna siku maendeleo yatakuja Tanzania. Kweli kwa mtindo huo ni ngumu sana.
   Juzi tumemsikia waziri mkuu anakataa gari ambalo limekwisha nunuliwa. Hivi huko serikalini hakuna mtu mwenye kauli moja ambaye akitoa basi waliopo chini yake wanatekeleza? Nauliza hivi kwa sababu ni muda mrefu sasa waziri mkuu alitamka kuwa magari ya bei kubwa na ya starehe yasinunuliwe na fedha hizo zielekezwe kununua matrekta madogo. Ilikuwaje wanunue aina ya gari la bei kubwa ambalo tayari waziri mkuu alishaagiza kutonunuliwa.
   Magari ya serikali yanatumika mitaani utafikiri ya watu binafsi. Hakuna anayekemea tabia hiyo. Mafuta yanayotumika siyo kodi ya wananchi. Kwa kweli ndugu zangu uzalendo wa nchi yetu umepungua sana. Hakuna anayemfikiria mtu wa chini sasa. Mmoja akishapata anawasahau kabisa wananchi wa chini.
   Ili Tanzania tuendelee tuwakute waliotuacha wakati tulianza pamoja, tunatakiwa kukaa chini kwanza tumtambue msaliti na huyo awe adui wetu sote tumuondoe na tujipange upya kwa mwendo mkali zaidi. Kama tutazidi kuwa naye huyu hata tujitahidi ataturudisha nyuma tu maana ni msaliti.
   Tutafika hapo tukiwaacha wananchi wawachague viongozi wao wanaowataka. Hakuna haja ya kulazimisha wananchi kupewa viongozi wasiowataka.

Wednesday, November 17, 2010

NYERERE FUFUKA UONE MAFISADI WAMEPOKA NCHI

Kwanza tuomba kuwasalimia Watanzania wenzangu!
Kwa kweli, naomba niyaseme yaliyomo moyoni mwaka maana nchi yetu inapelekwa kubaya.
Nakumbuka enzi hizo za utawala wa mzee Mwinyi kuna mambo yalitaka kujitokeza mwalimu akayakemea kwa nguvu zake zote. Leo yanatokea hakuna mtu wa kuyakemea. Wanyonge wasio na mtetezi wamebaki wanalia. Mafisadi wamekosa huruma,. Rushwa kila mahali.
Kwanza, Watanzania tujue kuwa matokeo ya uchaguzi yaliyotoka yanasemekana siyo yenyewe na kweli dalili zipo kwamba si yenyewe. Matokeo yamechakachuliwa na hivyo wananchi wamenyang'anywa haki ya kumchagua kiongozi wanayemtaka. Kama hali ndo hii ndugu zangu Tanzania yetu inaenda wapi?
Pili, Tanzania hakuna huduma inayotolewa bila kuwa na harufu ya rushwa. Popote unapoenda kupata huduma lazima uwe na chochote. Bila hivyo hakuna anayekujali. Watu sasa wanajali matumbo yao tu! Ubinafsi unatuua. Uongozi uliopo unaona lakini hakuna kinachosemwa kuhusu hayo mambo. Angalia wakati wa uchaguzi watu walitoa hela hadharani na hakuna aliyechukuliwa hatua maana watwala wenyewe walihusika. Uongozi umenunuliwa na wwatu wenye pesa na kama huna mfukoni shauri yako kafie mbali.
Tatu, udini umekuja kwa kasi ya ajabu. Watu sasa hawachagui viongozi kulingana na hoja walizo nazo wagombea ila huyu anasali wapi na ni muumini wa dini gani. Angalia wakati wa uchaguzi watu walivyohamasishana kuchagua waumini wenzao badala ya kuangalia kiongozi anayefaa. Tanzania leo hakuna mtu wa kukemea haya wazi wazi. Viongozi wakubwa wastafu hawana hata ubavu wa kukemea lakini wanayaona. Chukua mfano CCM walipokuwa wanafungakampeni zao rais mstaafu Benjamin William Mkapa alivyokanusha kuwepo kwa masuala ya udini wakati yapo kabisa na yanaonekana. Halafu mzee huyo aliwakandia viongozi wa dini kwa kusema kuwa wenyewe ndo wanaleta udini. Hiyo si kweli ila viongozi wakubwa wa kisiasa wameonesha kwa vitendo kabisa udini walio napo. Angalia teuzi mbalimbali za viongozi, mwelekeo ni udini haswa lakini mtu akisema eti ni mzushi. Jamani, nawaambieni nchi hii inakoenda siko. Tuchukue hatua. Demokrasia inaminywa.
Nne, kwa sasa ukiwa mtetezi wa wanyonge hapa Tanzania unaonekana hufai. Angalieni kilichotokea kwa mheshimiwa spika wa zamani wa bunge Sitta. Kwa kweli inasikitisha maana unapoona mzee kama yule aliyejitoa kuhakikisha bunge linakuwa mtetezi wa maslahi ya taifa anaonekana hafai tena, nani anfaa sasa? mafisadi wa nchi hi ndo wanafaa? Mimi nasema ujinga wetu Watanzania unatumaliza kabisa!
Tano, angalieni viongozi wastaafu wanasema nini. Kimya!! Mwalimu alipostafu alibaki kuwa mshauri, hivyo hata kama kuna jambo lilionekana kwenda visivyo, alikemea. Leo nani akemee maana akiona ananyamaza kwa kuwa usafi wake unatiliwa mashaka. Kwani nyie Mafisadi mnataka muwe naTsh ngapi ndugu zanguni? Mnasahau kuwa maisha hapa duniani hayazidi miaka mia moja? Kwa kweli MUNGU SAIDIA!!
Sita, ukionekana umejitokeza kutaka kusaidia maskini na watu wakikukubali, mafisadi wanakuja juu! Mafisadi wanataka kuendesha serikali. Jamani, mimi nalia. Tufanye nini ndugu zanguni! Mwalimu tunaomba ufufuke utusaidie tumebanwa kila kona! Hatuwezi kupumua!! Mfano, Dr. Slaa anaonekana kuja na mbinu mbadala kwa ajili ya kurekebisha hizi taabu za maisha wanazopata Watanzania. Baada ya kuona hivyo mafisadi wamekuja na kila uchafu wa kumbebesha mtu huyu! Hivi ina maana Tanzania uongozi ni wawateule fulani? Mbona mtu akitokea kuonekana anataka kuwashinda mnatumia mbinu chafu hata uongo wa kuzua ilimradi wananchi wamchukie? Ndugu, nchi hii imetekwa na mafisadi. Maskini hatuna chetu. Wattoto wa viongozi wanazunguka huku na huku wakitumia raslimali za wananchi ili mradi tu wazazi wao washinde kwenye chaguzi waendelee kula paradiso ya dunia!
Mwisho, enyi ndugu zangu Watanzania, mbona mmelala? Watu mliofikiri mnachagua wawakilishe, hawasimamii hoja zenu! Wakipewa cheo wanafanya kazi kwa maslahi ya wale waliowaweka. Hawaangalii maslahi ya watu. Mfano, hivi kulikuwa na sababu gani ya spika wa bunge kuanza kutoa tafsiri ya uongo ya neno "fisadi". Eti anafanya hivyo ili kumdhalilisha mtu fulani. Na kosa la mtu huyo tu ni kwa kuwa alitaka kunyang'anya kitumbua mdomoni mwao! Hivi ni lini hawa watu watawawakilisha wananchi. Majitambo yao eti wamekuwa uongozini toka miaka ya sabini. Bila aibu wanafikiri watu wanawashangilia na kufurahi. Miaka hiyo yote mmeoipeleka wapi nchi yetu hii? Jamani Watanzania tufanye nini hapa? Wabunge wetu wanampigia kura mtu ati kwa kuwa wako chama kimoja na siyo hoja alizonazo! Hivi hawa wabunge wetu wanafaa kweli? Watatusaidia nini. Malengo yao ni kusaidia watu au kuhakikisha wanalinda nafasi na kuongezewa nafasi nyingine kwa kuwalamba miguu viongozi wa chama chao!! Inatisha.
TUNATAKA MABADILIKO!!!
0753903809

Thursday, November 4, 2010

JE, UONEVU HUU MPAKA LINI?

Ndugu Watanzania wenzangu wapenda nchi yetu iliyotukuka!
Mungu wetu alipoiumba dunia hii alikusudia viumbe wake wote wafurahi bila kuoneana. Kwa kufuata msingi huu, katika katiba za makundi mbalimbali kuna maneno kama "BINADAMU WOTE NI SAWA".
Kutokana na ukweli huu, watu kwa kutumia akili zao kubwa wakatafuta mitindo mbalimbali ya namna ya kuweka serikali zao madarakani. Watu wengi kwa sasa wanapendelea mifumo ya kidemokrasia. Mfumo huu unapendwa zaidi kwa kuwa hushirikisha watu wote kwa namna moja au nyingine katika kutoa maamuzi yanahusu jamii hiyo.
Demokrasia maana yake "Utawala unaowekwa na watu". Hivyo ili nchi moja iitwe ni ya kidemokrasia, lazima serikali ya nchi hiyo iwe imewekwa na watu.
Ili kudumisha hali ya utengamano ambamo watu wanajisikia wamo katika nchi yao, lazima mambo mengi ya kijamii yafanywe kwa uwazi mkubwa na maamuzi yao yaheshimiwe sana.
Kutokana na ukweli huo, sisi Watanzania pia lazima tufuate utaratibu huu wa kidemokrasia ili tusiwe na manung'uniko katika nchi yetu sote. Pale panapotokea kundi moja dogo la watu waroho wa madaraka wanahodhi maamuzi ya watu na kufanya kila kitu kiwezekanacho kudidimiza matakwa ya watu wengine, basi nchi huishia katika vurugu kubwa sana ambayo kuizima huwa ni taabu kubwa sana.
Ndugu Watanzania, juzi tumekua na uchaguzi mkuu ambao ulitakiwa utupe madiwani, wabunge na rais tunayemtaka.
Kitu kinachosikitisha sana ni pale tunapoona kuna dalili za makusudi kabisa za kupotosha hali halisi ya matokeo ya uchaguzi huo.
Watu wanasema matokeo yanayotolewa si yale ambayo yapo kwenye vituo vya kupigia kura. YANABADILISHWA!! Hivi jamani mnataka watu watumie lugha ipi kupata haki yao?
Kama ni kweli matokeo hayo si yale yanayotakiwa yatolewe, kweli mimi binafsi kama Mtanzania wa nchi hii, naomba turudishe matokeo halisi ili sisi wapiga kura tujisikie tumesikilizwa na tujisikie tumo katika nchi yetu.
Ndugu zangu, uchaguzi ni gharama kubwa sana. Lakini kama baada ya uchaguzi anatangazwa yule aliyechaguliwa, uchaguzi huwa na maana sana na haijalishi gharama yake. Kama uchaguzi ni gelesha ili watu wapumbae na walio madarakani wabadilishe matokeo waonekane wao ndo wamechaguliwa wakati siyo, kweli inauma sana na kila mwenye uchungu na nchi hii anasikitika sana. "EE MUNGU WETU MBONA UMETUACHA?".
Enyi vingozi wa dini mnayaona haya? Enyi wazalendo wa nchi mnayaona haya? Mwalimu Nyerere tunaomba ufufuke uone yanayoendelea!!
Watu wachache wameiba mali ya taifa letu. Watu wanaliangamiza taifa hili, na bado wanang'ang'ania kubaki madarakani hata pale wapiga kura wanapowakataa. Tumesikia kuna wagombea wanaoshindwa wanadiriki hata kuhonga wale wanaoshinda watangaze wameshindwa! Hivi jamani sisi wenye ngozi nyeusi hata akili yetu ni nyeusi? Mambo tunayofanya si sahihi hata kidogo. Ni uonezi mkubwa.
Leo hii mimi nikipata ubalozi wa nyumba kumi basi na watoto wangu wote na mke wangu ni mabalozi. Nao wanaanza kutoa matamko ya kibalozi kwa wau wangu. Gharama za uendeshaji wa ubalozi wa nyumba kumi inaongezeka kwa kuwa ubalozi huu ni familia yote! Jamani tunaomba huruma sisi Watanzania wenzenu, mbona hivi jamani?
Kumwita mwenzako kokoto ati kwa sababu tu ameamua agombee nafasi ambayo wewe unagombea siyo sawa hata kidogo kwani si wewe tu una haki ya kufanya hivyo.
Kutumia mali za umma kuhadaa watu ambao bado elimu yao ndogo ili wakuchague badala ya kuunza sera ya namna utavyoleta unafuu wa maisha yao si sawa hata kidogo!
Eti nyie watu, mbona nashangaa sana! Unajisikia vipi unapolazimisha watu wakuchague au hata kuiba kura uonekane umeshinda wakati pengine hukushinda. KWANI TUNAPOSEMA SISI NI WAUMINI WA DINI FULANI HUWA HATUMAANISHI? Maana muumini wa kweli ni yule anayezingatia maagizo ya MWENYEZI MUNGU!
Ndugu zanguni, kwa kuwa hili si jambo la mchezo tuombe wenzetu wanaofikiri ndo wenye haki zaidi ya nchi hii waache mawazo hayo na watoe nafasi kwa wananchi waseme wanataka nini! Kama kweli kuna njama za kuiba kura njama hizo ziazhwe mara moja na kila mmoja apate kura halali alizopewa na wananchi.
MUNGU IBARIKI TANZANIA!!

Sunday, October 31, 2010

SAA YA UKOMBOZI IMEFIKA

Ndugu zangu Watanzania, inaonekana wengi wetu wamegundua kuwa nchi yetu ipo mikononi mwa mafisadi na hivyo tumeamua kuhakikisha kufanya jitihada ya kuikomboa nchi hii kutoka kwenye mikono michafu ya watu hawa wasio na huruma yoyote.
Kila kukicha wamekuwa wakipanda ndege kwenda nje ya nchi kunywa chai na bwana Obama. Wakiwa majukwaani watuambia wamepigiwa simu na Obama. Sisi simu za Obama hatuzihitaji ila tunachokitaka ni maendeleo. Wakiwa majukwaani wanaonyesha mbwembwe kwamba wanaweza sana kucheza na kunengua kumbe sisi hatuhitaji hayo ila maendeleo.
Ndugu zanguni, hatua hii si mbaya! Tumefika mahali na wala tusikate tamaa kabisa ukombozi umekaribia na tunaweza kurudisha nchi yetu mikononi mwetu. Sisi ni wapiganaji tusiochoka!
Katika historia hakuna mpiganaji yeyote aliyeungwa mkono kwa asilimia mia moja! HAPANA! cha msingi hapa ni kutokukata tamaa maana muda wa ukombozi umekaribia.
Hapa zamani walitudanganya kwa maneno matamu eti maisha bora kwa kila Mtanzania kumbe maana yake ni maisha bora kwa kila mwanafamilia ya bwana mkubwa. Ehee, jamani saa ya ukombozi imefika. Tusilale mpaka tuhakikishe nchi yetu ipo mikononi mwetu.
Kumbe mambo si haba! Mafisadi wanatetemeka na matumbo yao moto.
HATULALI MPAKA KIELEWEKE!!!

Tuesday, October 26, 2010

KILA MMOJA WETU AHAKIKISHE ANASHIRIKI KIKAMILIFU KUIKOMBOA NCHI YETU

Mwaka 1961 Tanganyika ilipata uhuru wa bendera kutoka kwa Waingereza. Ingawa tulio wengi hatukuwepo muda huo, tunajua kuwa wazee wetu walidai uhuru kwa madhumuni ya kuhakikisha tunajitawala ili tujifanyie mambo yetu tunayoyataka bila kushinikizwa na nyingine na pia kuona wananchi wanapata mamlaka ya kuendesha nchi yao.
Kwa hali hiyo kila Mtanganyika alikuwa na matumaini makubwa sana. Kwa hali ya kawaida binadamu ana mahitaji muhumu matatu. Nayo ni chakula, malazi na mavazi. Hivyo mtu yoyote utakayemwona anashughulika ujue yuko katika mchakato wa kuhakikisha anapata hayo mambo matatu bila shida.
Mungu alipomwumba mtu alitaka kila mmoja afaidike na raslimali za pale alipozaliwa. Kwa maana hiyo Mungu alikusudia Watanzania wafaidike na mali zao zilizopo Tanzania.
Ubinafsi ulipoanza, ndipo historia ya dhuluma ilipoanza. Tunasikia mambo ya biashara yalianza kila mtu akitafuta faida kwa kufanya dhuluma kwa mwenzake na hivyo hiyo ikaonekana kwamba ndani kwa kila mtu kuna kitu fulani kinachomssukuma kukusanya mali nyingi kwa kufanya wizi fulani. Hii haikuwa kusudi la Mungu!
Tabia hiyo ni mbaya sana tena nafikiri kwamba ubinafsi ni dhambi. Pale unapofanya dhuluma na hasa kama mtu umekabidhiwa mali ya jumuia wewe unakuwa ni muuaji sawa tu na yule anayechukua panga na kumkata mtu mwingine kwa ajili ya kunyang'anya mali.
Ndugu Watanzania, nchi yetu imetumbukia katika dimbwi kubwa la ubinafsi na wizi mkubwa sana. Viongozi wetu tuliowaamini na kuwapa dhamana wamejisahau na wamefikiri mali yote ni yao na hivyo hakuna haja ya kuwatumikia wananchi ila ni kuhakikisha wanafanya jitihada yoyote kuhakikisha wanashinda na wanabaki madarakani waendelee kuiba na kujinufaisha wenyewe.
Kama vile imesemwa mwanzo kwamba lengo la kudai uhuru kutoka kwa wale waliotangulia kuwa wabinafsi na kuja kututawala na kuiba mali zetu ilikuwa ni kuona mali zetu zinatufaidisha wote. Kitu cha ajabu ni kuwa baada ya kupata uhuru watu wamesahau malengo hayo na wanachofanya ni kuviziana na kila mmoja kunyakua kile kilichopo mbele yake na kuondoka.
Mambo haya yanadhihirika tunapoona viongozi wetu wanalimbikiza mali kupindukia wakati huo Watanzania wengi wakiwa hata hawawezi kupata yale mahitaji muhimu hata kwa kiwango cha chini kabisa.
Serikali yetu ya muhula wa nne imefanya mambo ya ajabu ya ubinafsi pengine kuliko serikali zote zilizotangulia. Hapa ninasema hivyo kwa sababu tumeona viongozi wetu wakiwa mahakamani kwa kesi za kukwapua mali za wananchi. Kitendo hicho ni kinyume kabisa na matarajio ya wengi.
Eti jamani, katika hali ya kawaida imewezekanaje mtu kupatikana na wizi huo lakini bado akaendelea kuwa katika ofisi ya umma na baadaye kupigiwa chapua la kuchaguliwa tena ili arudi katika nafasi ile ile aliyotumia kuiba mwanzoni?
Hivi sisi Watanzania hatuwezi kuona, kuhisi, kusikia wala kunusa!
Pengine tuseme hivi hatuwezi kuona haya yanayotendeka wazi wazi. Mtu anakuibia halafu baadaye anaomba umchague tena arudi madarakani kwa kukuletea komedi ili usahau lile alofanya mwanzo. Je, sisi Watanzania ni watu wa aina hiyo?
Ndugu zanguni, bila kuwa wanafiki mnajisikiaje pale familia moja inapotumia jasho la mlipa kodi ili kufanya mambo ya kifamilia yasiyo ya msingi kwa ustawi wa taifa letu. Mume ndege, mke ndege, watoto magari ya bei kali. Hizi ni mali za nani hasa.
Watanzania, kwa pamoja tuinuke tukapige kura ili tuwatose hao wasiotufaa.
Tuanze na kuona mali zetu zinavyoliwa na watu wachache wasio na uchungu na nchi yetu.
Mambo ya msingi yanayotakiwa yafanyike ili sisi tujikomboe na umaskini tulio nao ni kuwekenza katika elimu. Hii ina maana elimu ni ufunguo wa maisha. Mtu aliyeenda shule akasoma na kuelewa anaweza kupata chakula bora, malazi na mavazi safi. Kwa maana hiyo kama elimu ndio msingi wa maisha kila mtoto wa Mtanzania anatakiwa apewe elimu bora. Ili kuweza kutimiza hili utoaji elimu hautakiwi kuwa na vikwazo vingi tunavyoona sasa. wengi ni mashahidi wa ukweli kwamba watoto wa walala hoi wameishia darasa la saba si kwa sababu hawana uwezo wa kuendelea juu hapana ila ni kwa sababu ya kutokupata fursa ya kusoma kwa kuwa wazazi wao hakuweza kuwalipia ada na michango mingine. Hii ina maana uwezo wa kifedha ndo kikwazo kikubwa kwa maendeleo ya elimu nchini kwetu. Je, nani atbisha hilo? Kama tunakubaliana hapo, basi kwetu kiongozi anayetangaza elimu bure ndiye huyo anayetufaa sisi na si mwingine.
Kama nyumba ni sehemu ya mahitaji muhimu ya binadamu, ni kiongozi gani atakayetuwezesha sisi tujenge nyumba tuishi ili tuwe tumepata hitaji hilo la binadamu? Mimi nafikiri ni yule anayekumbuka hata kutuambia tu kwamba ujenzi wa nyumba utawezekana kama vifaa vya ujenzi vitakuwa vya bei ya chini ili wengi wetu tununue na tujenge nyumba. Kuongelea tu ujenzi wa barabara haitoshi maana barabara zinakumbukwa zaidi kwa kuwa hao wanaoiba na kufaidika kibinafsi na mali za nchi yetu ndo wenye magari ya kupitisha hizo barabara. Mimi mlala hoi cha msingi nyumba, elimu, na chakula. Barabara sawa lakini twende kwa vipau mbele ili kinachofanyika kimguse mwananchi wa chini kabisa.
Ili wananchi tuwe na nguvu ya kuleta serikali tunayotaka madarakani tunayo silaha moja kubwa: "KUPIGA KURA". Tusidanganywe ili tupige kura kumpigia mtu eti aliyetoa t-shirt, kofia na mabango. Mabango hayo ni fedha yetu inayotumika vibaya. Tunasema inatumika vibaya maana tungeondoa ubinafsi hiyo fedha iliyotumika kutengeneza mabango ingetununulia vitabu ili tusome tupate elimu bora.
Kwa kweli amini msiamini ndugu zangu, Tanzania yetu kwa sasa inahitaji matengenezo makubwa la sivyo huko tunako enda siko tuliko kusudia kwenda.

Thursday, October 21, 2010

TUACHE MAWAZO MGANDO

    Ndugu Watanzania wenzangu mnaoipenda nchi yetu, naomba wote kwa pamoja tufunge mikanda kuelimisha watu fulani ambao inaonekana mawazo yao ni ya zamani sana na inaonekana elimu waliyoipata waliipata kwa njia moja inayoitwa "indoctrination". Katika njia hii ya kupata uelewa fulani, mtu hupewa na kuaminishwa kitu fulani ambacho hicho atakisimamia mpaka hata afe lakini haachani nacho hata kidogo. Mtu huyo akiulizwa aeleze sababu za kung'ang'ana na hicho kitu mara nyingi haelezi vilivyo ila huishia kutetea na pengine ugomvi na yeyote anayekuwa tofauti naye katika mawazo.
    Jamani hivi inahitaji madarasa mangapi kuelewa kuwa duniani hapa wati hawafanani kwa sura na hata kwa mawazo? Inahitaji nini kujua kuwa kila binadamu hapa duniani ana kasoro zake ingawaje kuna tofauti katika uwingi wa kasoro kati ya mtu na mtu?
    Haya jamani. Jana magazeti yameandika kuwa Serikali inayatishia magazeti ya mwana Halisi na Mwananchi kuwa yatafungiwa sababu eti yanaichonganisha serikali na wananchi wake. AJABU! Hivi kusema kinyume na ulichopenda waseme ni uchonganishi? Kwa kweli ni ajabu kidogo. Ukiwa mtaani na ukakuta watu wamekaa wanaongea, utaona kuwa kila mtu anakuwa na wazo lake huyu hivi na yule vile. Sawa kwa kuwa hatufani!
     Magazeti hayo yaliyotajwa hayachonganishi ila nahisi mara nyingi yanaandika kile ambacho wakubwa wengi hawapendi kiandikwe. Hawapendi kiandikwe kwa kuwa hawajafanya kazi waliyotumwa na wananchi wakafanye. Wafikiria: Mbona magazeti haya yanaanika uovu wetu, tufanye nini kuyazima. Kama kweli magazeti haya yanaichonganisha serikali na wananchi ni habari ipi wameisema imechonganisha!!
Nawashauri serikali ifanye kile walichotumwa na wananchi waone magazeti yataandika nini. Hivi kama serikali imejenga daraja na inatoa elimu bure kwa wananchi na inashughulikia mafisadi ipasavyo kwa nguvu zote, itawezekana magazeti hayo kuandika kinyume na hapo kweli wakati matunda yanaonekana na wananchi wenye!HAPANA.
      Ili tuweze kumudu haya yote tunahitaji serikali safi. Usipokuwa msafi kila unakopita, kila unachosikia unalalama na kulalamika tu eti wananisema! TUAMKE.
      Pia kuna Watanzania mmoja mmoja wananichekesha sana. Hivi eti nyie watu hamuelewei kuwa mwalimu Nyerere naye alikuwa binadamu na kile alichoamini na kupigania si wote walikipokea? Kuna mtuwa ajabu na ajabu kweli na amenishangaza na kweli. Nasema amenishangaza kwa kuwa inaonekana ameenda shule lakini bado anaamini kuwa mtu yeyote aliyetofautiana na mwalimu Nyerere alau katika mfumo wa ujenzi wa taifa letu ni mdhambi kabisa na si tu wa kumfuata. Huyu jamaa amesoma lakini kichwani ana mawazo ya mgando kabisa.
   Mwalimu Nyerere, baba wa taifa letu, alifanya kazi kubwa sana kuikomboa tanganyika yetu toka kwa mkoloni na akatafuta mwelekeo wa taifa letu katika kukunza uchumi. Alijaribu na akafanikiwa kiasi fulani lakini pia yeye kama binadamu alishindwa hapa na pale na hili yeye mwenyewe anakiri hivyo.
   Kwa kuwa hakuwa malaika, kuna watu pia walioona mwelekeo aliochukua ulikuwa hauwaridhishi na hivyo hawakuwa pamoja naye kwa kila kitu kwa maana ya kuwa walikubaliana katika hili na wakatofautiana katika lile. Nani alikuwa sahihi, hilo hatujui!!
Tofauti hiyo haikumanisha kuwa watu waliotofautiana na mwalimu hawakuwa wazalendo, HAPANA. Walikuwa wazalendo tena wazuri kabisa na ndio maana wakajipambanua wakaonekana wametofautiana naye. Hivyo kwa mtu yeyote anayefikiri kutofautiana na mwalmu ilikuwa dhambi ana mawazo yaliyoganda kabisa.
     Huyu ndugu yetu Sheka ninamuomba atueleze zaidi kwa uwazi anachoona Mtei alikosa sana kwa kutokuwa pamoja na mwalimu katika mambo fulani kama kweli tofauti hiyo ilikuwepo. Je, babu yake Sheka hayupo katika historia ya ukombozi, hivyo tuseme hakuwa mzalendo? Hata kama Mtei hakushiriki kikamilifu katika mapambano ya kuikomboa Tanzania, kama ni kweli hivyo ndivyo, ni mawazo ya mbali sana kuona hilo linamwondolea haki ya kuanzisha chama. Kwani wote walowahi kushika madaraka walikuwepo wakati wa ukombozi miaka hiyo? SHEKA aachane na mawazo hayo. Labda kwa hayo aliyosema atuambie kwa uhakika masterpan ya CHADEMA ambayo sisi hatuifahamu ili tufahamu tupime. Lakini kama ni hiyo stori aliyokopi na kupesti, haijafanya chochote.http://www.mrmduda.blogspot.com
 

Saturday, October 16, 2010

HAKI NA AMANI


HAKI NA AMANI
  Haki na amani kwa namna moja au nyingine huitwa maneno pacha ingawa kila neno linaweza kuwa na maana tofauti na jingine.
  Neno haki kwa tafsiri au maana ya kawaida ni stahiki ya mtu kwa maana ya kile mtu astahilicho mtu kwa minajili ya kuwa binadamu au vinginevyo kama ilivyoainishwa katika jamii husika.
  Hii ni kusema kwamba zipo haki kama vile za kisiasa, kiuchumi, kijamii na nyingine nyingi kuendana na jamii yenyewe inavyoweza kuainisha kulingana na mahitaji katika jamii hiyo husika.
  Haki ya mtu au watu ikipokonywa au kuminywa mara moja hujibainisha kwamba hapa kuna jamba ambalo limekwenda kinyume. Madhara ya hili huwa kubwa kuliko hata gharama ya kuandaa haki hiyo.
  Ni madhila ya Haki ndiyo yanayotupatia Amani, kwamba palipo na Haki pana Amani. Kwa mantiki hii Amani ni zao la Haki. Neno amani lina dhana pan asana kwani inatiririka kutoka kwa mtummoja mmoja , kundi dogo la watu hadi jamii zima kwa ujumla wake.
  Kwa upande mwingine tunaweza kusema Haki huzaa imani na Imani huzaa Amani. Watu waliotendewa Haki, wasio na hofu Haki zao kufinyangwa, huwa na imani thabiti dhidi ya mamlaka zinazokabidhiwa jukumu la kutoa Haki hiyo.
  Hapa ndipo tunapoona upacha kati ya Haki na Amani, kwamba jamii iliyo na uhakika wa kupatiwa Haki zake itakuwa na Amani, na palipo na Amani ndipo maendeleo huwepo!
 Swali la kujiuliza hapa ni: je, jamii zetu zinapata Haki zake kwa kadri ya mahitaji yao? Amani ipo? Na kama ipo ni kwa kiwango gani? Kama haipo, ni kwa nini?
  Na je, kama wana jamii tunacho chochote cha kuchangia ili Haki na Amani viwepo? Tunashiriki vipi katika upatikanaji wake pasipo jamii kuparaganyika?
  Maswali yote haya na mengine mengi yanahitaji mjadala mpana kwa kila aliyepewa pumzi ya uhai na Mwanyezi Mungu kwa karama zake, wawe ni: wananzuoni au wanagenzi au wakurugenzi.
  Pengine kutokana na uzito na upana wa mjadala huu, ningependa niseme kila mmoja wetu ahusike ili tuweze kujifunza kwa pamoja na tuone jamii yetu inakwenda wapi na ipo katika hali ipi.
  Upo usemi usemao Haki yako inapoishia ndipo haki ya mwenzi inapoanzia
  Tujue kwamba kukosekana kwa Haki kumechangia sana kuongezeka kwa umaskini nchini mwetu.
  Fikiri kwa mfano, mwanafunzi wa elimu ya juu anahitaji mkopo. Katika fomu anayojanza, anatkiwa kugongewa mhuri mahakani.
  Anapofika mahakani anamkuta karani na kuambiwa kuwa inatakiwa igongwe mihuri sita na kila mhuri ni Tsh 1500. Huyu mwanafunzi anagongewa na hapewe risiti kuonyesha hiyo fedha inaingia kwenye mfuko wa nani.
  Au pia huyo mwanafunzi anashindwa kupata hiyo fedha na anaondoka. Na hivyo anaendelea kuhangaika maana bodi ya mikopo haitoi fedha kwa kuwa mwanafunzi huyo hakufanikiwa kigonga mhuri katika fomu huko mahakani. Je, huyu atakuwa na amani?
  Hivi ni nani alitakiwa ahakikishe kule mahakamani mambo yanaenda sawa. Siyo serkali yetu?
  Kwa kweli ndugu zangu pasipo na haki hakuna maendeleo yatakuwepo.
  Rushwa ikitawala, hakuna raia atapata haki yake. Hakuna mtu atakuwa na imani na mtawala wake.
Kinachohitajika hapa ni mabadiliko makubwa katika uendeshaji wa masuala ya umma. Kama kuna wakati mtu aliyeonwa na kashfa ya kuchukua rushwa anataka tena achaguliwe awe kiongozi, na anachaguliwa, hivi kweli watu wa jamii hiyo wataonekana makini katika mamabo yao au wanafanya mchezo!!
  Hapa ndipo mgogoro wa upatikanaji wa haki na Amani katika jamii zetu unapoanzia: kwamba waliokabidhiwa keki ya taifa ili waigawe kwa Haki, humegeanamegeana. Sehemu kubwa ya keki hiyo huichukua wao wenyewe kwa manufaa yao na familia zao.
  Nimalinze kwa kusema Haki na Amani si swala la utashi, ni la lazima ili tuweze kupata ustawi wa kweli wa jamii zetu ili kutimiza usemi usemao: “Dunia unaweza kuitafsiri utakavyo wewe, lakini kinachotakiwa ni maendeleo”.

Friday, October 1, 2010

HUDUMA YA ELIMU, AFYA KUTOLEWA BURE INAWEZEKANA

Watanzania tusidanganyike kuambiwa kupata huduma ya afya na elimu haiwezekani!
Watu wengi wanaotafuta nafasi mbalimbali kutuongoza katika taifa letu la Tanzania wanatuambia kuwa huduma hizo zinaweza kutolewa bure.
Watu wengine wanapinga sana hoja hizo. Mimi nasikitika kuona kuna watu wanapinga wakisema huduma hizo haziwezi kutolewa bure!
Kadri yangu mimi nahisi inawezekana.
Kwanza, wakati wa mwalimu Nyerere miaka hiyo vitu hivyo vilitolewa bure kabisa. Kama katika kipindi hicho mambo hayo yaliwezekana iweje leo isiwezekane. Watuambia kitu ambacho kinafanya huduma hizo ziweze kutolewa bure.
Pili, wakati wa mwalimu Nyerere hapakuwa na miradi mingi kiasi cha miradi iliyopo sasa. Kadri ya wenyewe wanasema uchumi umekua. Kama uchumi umekua ina maana sasa tunao uwezo zaidi kuliko wakati huo. Kama tunao uwezo wa kiuchumi zaidi kuliko wakati huo, basi tunao uwezo zaidi wa kutoa huduma bure kuliko wakati ule.
Tatu, ufisadi mkubwa uliotokea katika nchi yetu unaashiria kwamba mali nyingi sana za nchi yetu zimefanya watu wengi tuamini kuwa kama pangekuwa na uaminifu katika serikali na ulinzi mahsusi wa mali za umma, basi watanzania wengi wangeamini kuwa huduma nyingi zaidi zenyi ubora zaidi zingewafikia Watanzania wengi zaidi.
Nne, misamaha ya kodi kwa wafanya biashara wakubwa inaonesha kuwa serikali haikusanyi mapato kwa makini zaidi ili kuhakikisha ina boresha huduma za jamii na pengine kuleta uwezekano wa kutoA HUDUMA HIZO BURE!
Tano, uzembe katika uimarishaji wa miundo mbinu yetu kwa ajili ya kukuza biashara zetu na nchi jirani unafanya watu waone kutoa huduma hizi bure haziwezekni! Kama tungeimarisha biashara yetu ya nje pato letu la taifa lingeongezeka sana na hivyo kuifanya serikali yetu iwe na uwezo wa kutoa huduma za kijamii bure.
Ukiangalia kwa makini sana utaona kuwa kutokuweza kufanya hivyo kunategemea sana watendaji wa serikali yetu waliopo madarakani. Kama wangejitoa kwa moyo wote kuwatumia wananchi mambo hayo yangewezekana.
Ili kuhakikisha tunakuwa na uwezo wa kupata huduma hizo za msingi bure, hatuna budi tudhamirie kweli tarehe 31-10-2010 tukapige kura na kuchagua viongozi wenye uwezo na mwelekeo chanya wa kuwatumikia wananchi kwa kuachana na viongozi mafisadi, wasio na uwezo wa kuona mbali na wenye ubinafsi ili wote na vizazi vyetu baadaye tufaidi matunda ya nchi yetu.

Friday, September 24, 2010

HIVI NCHI YETU NI KILEMA!

Wakati akipiga kampeni jana, mgombea wa kiti cha urais kupitia chama cha mapinduzi, Mheshimiwa Dr. Jakaya Mrisho Kikwete alipigiwa simu na balozi wa Marekani hapa Tanzania. Baada ya kumaliza kuongea na huyo balozi, Mheshimiwa rais aliwaambia wananchi waliokuwa wanamsikiliza kuwa kupitia kwa balozi Obama, rais wa Marekani ameahidi kuendelea kutoa misaada Tanzania kwa sababu Tanzania inazingatia misingi ya uongozi bora.
 Kwa kweli mimi sikutegemea kabisa!
 Ndugu zanguni Watanzania, hivi nchi yetu ni kilema kweli kiasi cha hata rais wa nchi kuchekelea hawa mabepari wakubwa wanapoahidi kutoa misaada?
 Naomba sana tukumbuke kuwa Wazungu huwa hawatoi chochote pasipo faida kwao. Wazungu hawa ni wajanja wa muda mrefu sana. Kila wanachofanya kwetu sisi Waafrika, hukifanya kama mtego wa kutunasa wachukue kila kitu ambacho kina faida kwao.
 Wazungu hawa walianza kutuibia zamani sana. Hawa huiba vitu vingi kwa ujanja sana. Miaka ya zamani sana walitufanya sisi wanyama wakawa wanatuunza. Wametunyonya kama watumwa kwa miaka.Walipoona biashara ya utumwa haina faida kama mwanzo, wakatutawala kama wakoloni.
 Ukoloni huo umekwenda kwa miaka mingi tukinyonywa katika mambo mengi sana. Walitufanyisha kazi mashambani mwao tuzalishe malighafi kwa ajili ya viwanda vyao. Baada ya miaka mingi ya kujiimarisha, wakaamua kutupa uhuru wa bendera wakituacha kwenye uchumi tegemezi ambao haukuturusu kujitegemea kabisa.
 Baada ya hapo kukaja ukoloni mamboleo. Katika ukoloni mamboleo, mtumwa mwinyewe analima, anatunza, halafu mkoloni mamboleo anakuja anakupanga bei ya mazao yako na wewe unasema ndiyo. Mkoloni akipata fedha  kutokana na mazao aliyonyang'anya, kiasi kidogo cha fedha anakupa na anaita ni msaada. Hicho kiasi chako kidogo cha dhuluma kinachokuja kwako mkoloni mamboleo anakiita msaada. Mkoloni mamboleo anatoa kiasi hicho ili kudumisha uhusiano mzuri kati ya mnyonyaji na mnyonywaji.
 Katika nchi ambamo hata kiongozi wa nchi anachekelea kupewa hicho kiasi kinachoitwa msaada, hakutakuwa na maendeleo hata siku moja.
 Kwa hiyo ndugu zangu Watanzania, tusijivunie kuona mheshimiwa Kikwete anaongea na balozi wa Marekani akiahidiwa kitu kinachoitwa misaada, hapo wanaweka mikakati ya kuendeleza hali yetu ya kunyonywa! Jana kuona vile ilitakiwa tusikitike siyo kufurahi na rais alitakiwa asijigambe kwamba tunaahidiwa kitu kinachoitwa misaada.
 Hapo alitakiwa baada ya kuongea tu, aseme, jamani mnaona unyonge tulionao? halafu kinachofuata alitakiwa awaambie wananchi namna alivyojipanga kuondoa hali duni na nyonge tuliyonayo kwa kutumia vizuri raslimali zetu hapa nchini.
 Watanzania tubadilike!!! TUWEKE MIKAKATI YA KUJITOA KWENYE MAKUCHA HAYA YA WAZUNGU. TUKATAE UFISADI maana huo ndo unaowakaribisha wazungu waje kuchukua madini yetu kwa bei ya kutupa maana kwetu ni shamba la bibi. Waangalizi wa shamba hilo ndo hao mafisadi. Mafisadi hao wanachukua chao mapema na makapi wanampelekea bibi. Bibi hajui kunachoendelea shambani kwa kuwa miguu yake ni midhaifu hawezi kufika shambani kwa kutembea.
 Unapofika wakati hawa mafisadi tuwaondoe jamani, hawafai. Tuwapeleke wengine ambao hawana tabia ya kifisadi!www.facebook/Expedito Mduda

Wednesday, September 22, 2010

TRUTH

Expedito Mduda
Truth is a concept in philosophy that treats both the meaning of the word true and the criteria by which we judge the truth or falsity in spoken and written statements. Philosophers have attempted to answer the question “What is truth?” for thousands of years. The four main theories they have proposed to answer this question are the correspondence, pragmatic, coherence, and deflationary theories of truth.
One of the earliest versions of the correspondence theory was put forward in the 4th century bc by the Greek philosopher Plato, who sought to understand the meaning of knowledge and how it is acquired. Plato wished to distinguish between true belief and false belief. He proposed a theory based on intuitive recognition that true statements correspond to the facts—that is, agree with reality—while false statements do not. In Plato’s example, the sentence “Theaetetus flies” can be true only if the world contains the fact that Theaetetus flies. However, Plato—and much later, 20th-century British philosopher Bertrand Russell—recognized this theory as unsatisfactory because it did not allow for false belief. Both Plato and Russell reasoned that if a belief is false because there is no fact to which it corresponds, it would then be a belief about nothing and so not a belief at all. Each then speculated that the grammar of a sentence could offer a way around this problem. A sentence can be about something (the person Theaetetus), yet false (flying is not true of Theaetetus). But how, they asked, are the parts of a sentence related to reality? One suggestion, proposed by 20th-century philosopher Ludwig Wittgenstein, is that the parts of a sentence relate to the objects they describe in much the same way that the parts of a picture relate to the objects pictured. Once again, however, false sentences pose a problem: If a false sentence pictures nothing, there can be no meaning in the sentence.
In the late 19th-century American philosopher Charles S. Peirce offered another answer to the question “What is truth?” He asserted that truth is that which experts will agree upon when their investigations are final. Many pragmatists such as Peirce claim that the truth of our ideas must be tested through practice. Some pragmatists have gone so far as to question the usefulness of the idea of truth, arguing that in evaluating our beliefs we should rather pay attention to the consequences that our beliefs may have. However, critics of the pragmatic theory are concerned that we would have no knowledge because we do not know which set of beliefs will ultimately be agreed upon; nor are there sets of beliefs that are useful in every context.
A third theory of truth, the coherence theory, also concerns the meaning of knowledge. Coherence theorists have claimed that a set of beliefs is true if the beliefs are comprehensive—that is, they cover everything—and do not contradict each other.
Other philosophers dismiss the question “What is truth?” with the observation that attaching the claim “it is true that” to a sentence adds no meaning. However, these theorists, who have proposed what are known as deflationary theories of truth, do not dismiss such talk about truth as useless. They agree that there are contexts in which a sentence such as “it is true that the book is blue” can have a different impact than the shorter statement “the book is blue.” More importantly, use of the word true is essential when making a general claim about everything, nothing, or something, as in the statement “most of what he says is true.”

NCHI YETU

 Ndugu zangu Watanzania, wapenda maendeleo wote, mwasisi wa taifa hili walimu Julius Kambarage Nyerere alipokuwa akiwahutubia waandishi wa habari wa hapa nchini wa kigeni Machi 14, 1995, alishutumu sana serikali ya aliyekuwa Rais wa nchi wakati huo, Rais Alli Hassan Mwinyi, kwa sababu ya ufisadi na uvunjaji wa katiba ya nchi.
 Katika hotuba yake ambayo aliitoa katika hotel ya kimataifa ya Kilimanjaro, mwalimu alishutumu serikali ya mrithi wake Mwinyi kwa kufumbia macho suala la udini na ukabila, na kudiriki kuwaasa Watanzania kuwa makini katika kuchagua serikali mpya ambapo ilikuwa imesalia miezi saba tu kufikia uchaguzi mkuu.
 Mwalimu aliendelea kuonya kuwa ikiwa Watanzania watakubali kuendekeza udhaifu wa aina hii, basi muungano wetu utakuwa hatarini na kupelekea kutetereka kwa amani nchini.
 Aliwatatahadharisha Watanzania kwamba wamchague mtu mwenye uwezo wa kurekebisha mambo, na kuirudisha nchi katika mstari ulionyooka.
 Je, Watanzania wenzangu, leo sisi tunasemaje? Mambo yote yapo swari? Kama kuna shida yoyote, basi huu ni muda mzuri wa kutumia kura yako kuondoa kasoro yoyote katika uongozi unaofuata sasa. Tuwanyime kura wote wale ambao ni wabinafsi, mafisadi na wasiowatakia mema Watanzania.Leo hii mwalimu angekuwepo angesema mengi zaidi maana nchi yetu sasa imetumbukia kubaya.
 Mijadala bungeni imejaa masuala ya ufisadi. Mafisadi hawa tumewachagua sisi wenyewe. Mimi nafikiri hakuna haja tena ya kuchagua watu wanaonuka uchafu huo.

Monday, September 13, 2010

KUMBE TUAMKE

  Zamani sana nilifikiri kila anayegombea uongozi ni mtu anayetaka kutumikia wananchi. Sasa ni mtu mzima nimeelewa kuwa watu wengi wanagombea uongozi kutafuta maslahi binafsi.
  Kwa mtu wa kawaida inakuwa ngumu kuingia akilini kwamba mgombea anakuja na kuahidi kufanya mambo fulani katika kipindi chake cha uongozi, lakini anapopata haonekani tena mpaka siku atakapoona siku za uongozi wake zinafika ukingoni.
  Ndugu, nchi hii ni yetu. Tuamke tuchague viongozi wanaoweza kutupeleka kule tunakotaka kwenda! Hatuwataki viongozi walafi, wanaotaka kulimbikiza mali wakati wananchi wanakufa njaa, wanakosa elimu, huduma za afya na mengineyo!
TUAMKE!!!!

Saturday, September 4, 2010

AFTER 31st OCTOBER

I am sorry for all those who have lost. It's an experience I (you) never had


Margaret Thatcher (1925 - )

.

Friday, September 3, 2010

TUNADANGANYANA SANA

               Habari ndugu zangu Watanzania wenzangu mliopendelewa kwani  mmejaliwa maliasili nyingi sana na MWENYE-MUNGU. Hivi zamani hapo wakubwa zetu walipokuwa bado wapo shule walipokuwa wanafanya kazi za mikono huko shuleni walipungukiwa au walipata maarifa zaidi?
Siku hizi watoto wakifundishwa kazi za mikono shuleni wanasema wanaonewa maana wanasema hawakufika shule kufanya kazi za mikono,
             Lakini pia wakiachwa wasome, hawasomi maana wanaishia kusema wanatafuta "credit". Ndugu zanguni, naomba sana tukae chini tuone ni aina gani ya kizazi tunataka kujenga. Tujiulize ni maarifa gani tungependa tupate.
Mimi nafikiri mtoto anapomaliza darasa la saba awe na uwezo wa kuzalisha shambani au katika sekta yoyote anayo bahatika kuwa nayo. Kama tutaacha watoto hawa wamalize shule wakati hawaelewi hata namna ya kutengeneza mahali pa kupanda sukuma wiki, tunatengeza bomu la nyuklia.

xxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxx

SIFA ZA ANAYETAKIWA KUTUONGOZA WATANZANIA

Ndugu zangu, hivi ni zipi sifa za kiongozi tunayemtaka?
Mimi nafikiri kiongozi anayetakiwa Tanzania ni yule anayetanguliza maslahi ya wananchi mbele. Siyo yule anayefikiri kulimbikiza mali wakati wananchi wake wanahangaika.
Ndugu wananchi wenzangu, hivi sisi ni vipofu kiasi kwamba tunaweza kumchagua mtu kwa sababu labda wakati wa kukampeni alikuja na ngoma za kienyeji au palikuwa na mdundiko? Hapana, sisi si vipofu kiasi hicho! Macho yetu yasiwe kifuani, yawe kichwani.
Kwani mnataka nani awaongoze? Si yule aliyefanya mengi kuwatetea wanyonge! Hivi ndugu zangu kuna haja sana ya kuambiwa nani kavulunda na nani kaonekana anaweza akafanya zaidi?
Ombi langu kwa Watanzania wapenda nchi yao, ni kuchagua viongozi wachapa kazi watakao tetea maslahi yetu siyo wanaojaza matumbo yao bila kujali wengine wanakufa au wanaishi maisha ya ajabu sababu tu miundombinu ya uchumi hairuhusu maendeleo.

DEMOCRACY

All the ills of democracy can be cured by more democracy.


Al Smith
(1873 - 1944)


Saturday, July 17, 2010

UCHAGUZI MWAKA 2010

Ndugu zangu waTanzania wapenda nchi yetu, nawaombeni sana sisi sote kwa pamoja tukumbuke kuwa mwaka huu ni mwaka wa uchaguzi mkuu.
Mstakabali wa nchi yetu ipo mikononi mwetu. Maendeleo ya nchi yetu yanatutegemea sisi.
Nawaombeni sana mkumbuke kuwa tunatakiwa tuchague viongozi watakaotufaa. Tunataka viongozi watakao kuwa chachu ya maendeleo. Viongozi wanaochukua chao mapema na kuondoka hatuwataki kabisa.
Mwaka huu ni wakati mwafaka wa kunyang'anya dhima ya uongozi tuliyowapa wale wote ambao hawajatekeleza yale waliyoahidi. Hivi jamani kuwa kiongozi ni kuwa bosi kwa wale walokupa dhamana hiyo?
Je, uongozi katika nchi yetu ni ya wale tu waliotuibia mali zetu na kujidai kuwa wao ndo watafutaji wazuri kuliko wengine?
Jamani mimi naomba tubalike wote kwa pamoja ili kuifanya nchi yetu isonge mbele. Mtu yeyote anaweza kuwa kiongozi ili mradi tu awe na nia ya kuwatumikia wananchi wenzake. Kuwa kiongozi maana yake kuwa na uwezo wa kuonesha njia na siyo kuwa na kujisikia bosi fulani.
Naombeni wananchi wenzangu tushirikiane kuwang'oa wale wote walotudanganya mwaka 2005 na tuwaweke wale tunaofikiri wana nia njema na nchi yetu na siyo wale mafisadi.
Tukumbuke kuwa uongozi siyo mali ya mtu binafsi.
Tarehe 31 -10 -2010 iwe ni siku ya mageuzi na isiwe ni siku ya kuwapa mafisadi ulaji.
Asanteni!