image slider

HUDUMA TUNAZOZITOA
Watengenezaji wa mashine za kuangulia vifaranga vya kuku
Wauzaji wa vifaranga vya kuku
Ushauri wa ufugaji wa kuku
Mashine za kuangulia vifaranga vya kuku
Wauzaji wa vifaranga vya kuku
Mashine za kuangulia vifaranga vya kuku

Friday, September 24, 2010

HIVI NCHI YETU NI KILEMA!

Wakati akipiga kampeni jana, mgombea wa kiti cha urais kupitia chama cha mapinduzi, Mheshimiwa Dr. Jakaya Mrisho Kikwete alipigiwa simu na balozi wa Marekani hapa Tanzania. Baada ya kumaliza kuongea na huyo balozi, Mheshimiwa rais aliwaambia wananchi waliokuwa wanamsikiliza kuwa kupitia kwa balozi Obama, rais wa Marekani ameahidi kuendelea kutoa misaada Tanzania kwa sababu Tanzania inazingatia misingi ya uongozi bora.
 Kwa kweli mimi sikutegemea kabisa!
 Ndugu zanguni Watanzania, hivi nchi yetu ni kilema kweli kiasi cha hata rais wa nchi kuchekelea hawa mabepari wakubwa wanapoahidi kutoa misaada?
 Naomba sana tukumbuke kuwa Wazungu huwa hawatoi chochote pasipo faida kwao. Wazungu hawa ni wajanja wa muda mrefu sana. Kila wanachofanya kwetu sisi Waafrika, hukifanya kama mtego wa kutunasa wachukue kila kitu ambacho kina faida kwao.
 Wazungu hawa walianza kutuibia zamani sana. Hawa huiba vitu vingi kwa ujanja sana. Miaka ya zamani sana walitufanya sisi wanyama wakawa wanatuunza. Wametunyonya kama watumwa kwa miaka.Walipoona biashara ya utumwa haina faida kama mwanzo, wakatutawala kama wakoloni.
 Ukoloni huo umekwenda kwa miaka mingi tukinyonywa katika mambo mengi sana. Walitufanyisha kazi mashambani mwao tuzalishe malighafi kwa ajili ya viwanda vyao. Baada ya miaka mingi ya kujiimarisha, wakaamua kutupa uhuru wa bendera wakituacha kwenye uchumi tegemezi ambao haukuturusu kujitegemea kabisa.
 Baada ya hapo kukaja ukoloni mamboleo. Katika ukoloni mamboleo, mtumwa mwinyewe analima, anatunza, halafu mkoloni mamboleo anakuja anakupanga bei ya mazao yako na wewe unasema ndiyo. Mkoloni akipata fedha  kutokana na mazao aliyonyang'anya, kiasi kidogo cha fedha anakupa na anaita ni msaada. Hicho kiasi chako kidogo cha dhuluma kinachokuja kwako mkoloni mamboleo anakiita msaada. Mkoloni mamboleo anatoa kiasi hicho ili kudumisha uhusiano mzuri kati ya mnyonyaji na mnyonywaji.
 Katika nchi ambamo hata kiongozi wa nchi anachekelea kupewa hicho kiasi kinachoitwa msaada, hakutakuwa na maendeleo hata siku moja.
 Kwa hiyo ndugu zangu Watanzania, tusijivunie kuona mheshimiwa Kikwete anaongea na balozi wa Marekani akiahidiwa kitu kinachoitwa misaada, hapo wanaweka mikakati ya kuendeleza hali yetu ya kunyonywa! Jana kuona vile ilitakiwa tusikitike siyo kufurahi na rais alitakiwa asijigambe kwamba tunaahidiwa kitu kinachoitwa misaada.
 Hapo alitakiwa baada ya kuongea tu, aseme, jamani mnaona unyonge tulionao? halafu kinachofuata alitakiwa awaambie wananchi namna alivyojipanga kuondoa hali duni na nyonge tuliyonayo kwa kutumia vizuri raslimali zetu hapa nchini.
 Watanzania tubadilike!!! TUWEKE MIKAKATI YA KUJITOA KWENYE MAKUCHA HAYA YA WAZUNGU. TUKATAE UFISADI maana huo ndo unaowakaribisha wazungu waje kuchukua madini yetu kwa bei ya kutupa maana kwetu ni shamba la bibi. Waangalizi wa shamba hilo ndo hao mafisadi. Mafisadi hao wanachukua chao mapema na makapi wanampelekea bibi. Bibi hajui kunachoendelea shambani kwa kuwa miguu yake ni midhaifu hawezi kufika shambani kwa kutembea.
 Unapofika wakati hawa mafisadi tuwaondoe jamani, hawafai. Tuwapeleke wengine ambao hawana tabia ya kifisadi!www.facebook/Expedito Mduda

Wednesday, September 22, 2010

TRUTH

Expedito Mduda
Truth is a concept in philosophy that treats both the meaning of the word true and the criteria by which we judge the truth or falsity in spoken and written statements. Philosophers have attempted to answer the question “What is truth?” for thousands of years. The four main theories they have proposed to answer this question are the correspondence, pragmatic, coherence, and deflationary theories of truth.
One of the earliest versions of the correspondence theory was put forward in the 4th century bc by the Greek philosopher Plato, who sought to understand the meaning of knowledge and how it is acquired. Plato wished to distinguish between true belief and false belief. He proposed a theory based on intuitive recognition that true statements correspond to the facts—that is, agree with reality—while false statements do not. In Plato’s example, the sentence “Theaetetus flies” can be true only if the world contains the fact that Theaetetus flies. However, Plato—and much later, 20th-century British philosopher Bertrand Russell—recognized this theory as unsatisfactory because it did not allow for false belief. Both Plato and Russell reasoned that if a belief is false because there is no fact to which it corresponds, it would then be a belief about nothing and so not a belief at all. Each then speculated that the grammar of a sentence could offer a way around this problem. A sentence can be about something (the person Theaetetus), yet false (flying is not true of Theaetetus). But how, they asked, are the parts of a sentence related to reality? One suggestion, proposed by 20th-century philosopher Ludwig Wittgenstein, is that the parts of a sentence relate to the objects they describe in much the same way that the parts of a picture relate to the objects pictured. Once again, however, false sentences pose a problem: If a false sentence pictures nothing, there can be no meaning in the sentence.
In the late 19th-century American philosopher Charles S. Peirce offered another answer to the question “What is truth?” He asserted that truth is that which experts will agree upon when their investigations are final. Many pragmatists such as Peirce claim that the truth of our ideas must be tested through practice. Some pragmatists have gone so far as to question the usefulness of the idea of truth, arguing that in evaluating our beliefs we should rather pay attention to the consequences that our beliefs may have. However, critics of the pragmatic theory are concerned that we would have no knowledge because we do not know which set of beliefs will ultimately be agreed upon; nor are there sets of beliefs that are useful in every context.
A third theory of truth, the coherence theory, also concerns the meaning of knowledge. Coherence theorists have claimed that a set of beliefs is true if the beliefs are comprehensive—that is, they cover everything—and do not contradict each other.
Other philosophers dismiss the question “What is truth?” with the observation that attaching the claim “it is true that” to a sentence adds no meaning. However, these theorists, who have proposed what are known as deflationary theories of truth, do not dismiss such talk about truth as useless. They agree that there are contexts in which a sentence such as “it is true that the book is blue” can have a different impact than the shorter statement “the book is blue.” More importantly, use of the word true is essential when making a general claim about everything, nothing, or something, as in the statement “most of what he says is true.”

NCHI YETU

 Ndugu zangu Watanzania, wapenda maendeleo wote, mwasisi wa taifa hili walimu Julius Kambarage Nyerere alipokuwa akiwahutubia waandishi wa habari wa hapa nchini wa kigeni Machi 14, 1995, alishutumu sana serikali ya aliyekuwa Rais wa nchi wakati huo, Rais Alli Hassan Mwinyi, kwa sababu ya ufisadi na uvunjaji wa katiba ya nchi.
 Katika hotuba yake ambayo aliitoa katika hotel ya kimataifa ya Kilimanjaro, mwalimu alishutumu serikali ya mrithi wake Mwinyi kwa kufumbia macho suala la udini na ukabila, na kudiriki kuwaasa Watanzania kuwa makini katika kuchagua serikali mpya ambapo ilikuwa imesalia miezi saba tu kufikia uchaguzi mkuu.
 Mwalimu aliendelea kuonya kuwa ikiwa Watanzania watakubali kuendekeza udhaifu wa aina hii, basi muungano wetu utakuwa hatarini na kupelekea kutetereka kwa amani nchini.
 Aliwatatahadharisha Watanzania kwamba wamchague mtu mwenye uwezo wa kurekebisha mambo, na kuirudisha nchi katika mstari ulionyooka.
 Je, Watanzania wenzangu, leo sisi tunasemaje? Mambo yote yapo swari? Kama kuna shida yoyote, basi huu ni muda mzuri wa kutumia kura yako kuondoa kasoro yoyote katika uongozi unaofuata sasa. Tuwanyime kura wote wale ambao ni wabinafsi, mafisadi na wasiowatakia mema Watanzania.Leo hii mwalimu angekuwepo angesema mengi zaidi maana nchi yetu sasa imetumbukia kubaya.
 Mijadala bungeni imejaa masuala ya ufisadi. Mafisadi hawa tumewachagua sisi wenyewe. Mimi nafikiri hakuna haja tena ya kuchagua watu wanaonuka uchafu huo.

Monday, September 13, 2010

KUMBE TUAMKE

  Zamani sana nilifikiri kila anayegombea uongozi ni mtu anayetaka kutumikia wananchi. Sasa ni mtu mzima nimeelewa kuwa watu wengi wanagombea uongozi kutafuta maslahi binafsi.
  Kwa mtu wa kawaida inakuwa ngumu kuingia akilini kwamba mgombea anakuja na kuahidi kufanya mambo fulani katika kipindi chake cha uongozi, lakini anapopata haonekani tena mpaka siku atakapoona siku za uongozi wake zinafika ukingoni.
  Ndugu, nchi hii ni yetu. Tuamke tuchague viongozi wanaoweza kutupeleka kule tunakotaka kwenda! Hatuwataki viongozi walafi, wanaotaka kulimbikiza mali wakati wananchi wanakufa njaa, wanakosa elimu, huduma za afya na mengineyo!
TUAMKE!!!!

Saturday, September 4, 2010

AFTER 31st OCTOBER

I am sorry for all those who have lost. It's an experience I (you) never had


Margaret Thatcher (1925 - )

.

Friday, September 3, 2010

TUNADANGANYANA SANA

               Habari ndugu zangu Watanzania wenzangu mliopendelewa kwani  mmejaliwa maliasili nyingi sana na MWENYE-MUNGU. Hivi zamani hapo wakubwa zetu walipokuwa bado wapo shule walipokuwa wanafanya kazi za mikono huko shuleni walipungukiwa au walipata maarifa zaidi?
Siku hizi watoto wakifundishwa kazi za mikono shuleni wanasema wanaonewa maana wanasema hawakufika shule kufanya kazi za mikono,
             Lakini pia wakiachwa wasome, hawasomi maana wanaishia kusema wanatafuta "credit". Ndugu zanguni, naomba sana tukae chini tuone ni aina gani ya kizazi tunataka kujenga. Tujiulize ni maarifa gani tungependa tupate.
Mimi nafikiri mtoto anapomaliza darasa la saba awe na uwezo wa kuzalisha shambani au katika sekta yoyote anayo bahatika kuwa nayo. Kama tutaacha watoto hawa wamalize shule wakati hawaelewi hata namna ya kutengeneza mahali pa kupanda sukuma wiki, tunatengeza bomu la nyuklia.

xxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxx

SIFA ZA ANAYETAKIWA KUTUONGOZA WATANZANIA

Ndugu zangu, hivi ni zipi sifa za kiongozi tunayemtaka?
Mimi nafikiri kiongozi anayetakiwa Tanzania ni yule anayetanguliza maslahi ya wananchi mbele. Siyo yule anayefikiri kulimbikiza mali wakati wananchi wake wanahangaika.
Ndugu wananchi wenzangu, hivi sisi ni vipofu kiasi kwamba tunaweza kumchagua mtu kwa sababu labda wakati wa kukampeni alikuja na ngoma za kienyeji au palikuwa na mdundiko? Hapana, sisi si vipofu kiasi hicho! Macho yetu yasiwe kifuani, yawe kichwani.
Kwani mnataka nani awaongoze? Si yule aliyefanya mengi kuwatetea wanyonge! Hivi ndugu zangu kuna haja sana ya kuambiwa nani kavulunda na nani kaonekana anaweza akafanya zaidi?
Ombi langu kwa Watanzania wapenda nchi yao, ni kuchagua viongozi wachapa kazi watakao tetea maslahi yetu siyo wanaojaza matumbo yao bila kujali wengine wanakufa au wanaishi maisha ya ajabu sababu tu miundombinu ya uchumi hairuhusu maendeleo.

DEMOCRACY

All the ills of democracy can be cured by more democracy.


Al Smith
(1873 - 1944)