image slider

HUDUMA TUNAZOZITOA
Watengenezaji wa mashine za kuangulia vifaranga vya kuku
Wauzaji wa vifaranga vya kuku
Ushauri wa ufugaji wa kuku
Mashine za kuangulia vifaranga vya kuku
Wauzaji wa vifaranga vya kuku
Mashine za kuangulia vifaranga vya kuku

Sunday, October 31, 2010

SAA YA UKOMBOZI IMEFIKA

Ndugu zangu Watanzania, inaonekana wengi wetu wamegundua kuwa nchi yetu ipo mikononi mwa mafisadi na hivyo tumeamua kuhakikisha kufanya jitihada ya kuikomboa nchi hii kutoka kwenye mikono michafu ya watu hawa wasio na huruma yoyote.
Kila kukicha wamekuwa wakipanda ndege kwenda nje ya nchi kunywa chai na bwana Obama. Wakiwa majukwaani watuambia wamepigiwa simu na Obama. Sisi simu za Obama hatuzihitaji ila tunachokitaka ni maendeleo. Wakiwa majukwaani wanaonyesha mbwembwe kwamba wanaweza sana kucheza na kunengua kumbe sisi hatuhitaji hayo ila maendeleo.
Ndugu zanguni, hatua hii si mbaya! Tumefika mahali na wala tusikate tamaa kabisa ukombozi umekaribia na tunaweza kurudisha nchi yetu mikononi mwetu. Sisi ni wapiganaji tusiochoka!
Katika historia hakuna mpiganaji yeyote aliyeungwa mkono kwa asilimia mia moja! HAPANA! cha msingi hapa ni kutokukata tamaa maana muda wa ukombozi umekaribia.
Hapa zamani walitudanganya kwa maneno matamu eti maisha bora kwa kila Mtanzania kumbe maana yake ni maisha bora kwa kila mwanafamilia ya bwana mkubwa. Ehee, jamani saa ya ukombozi imefika. Tusilale mpaka tuhakikishe nchi yetu ipo mikononi mwetu.
Kumbe mambo si haba! Mafisadi wanatetemeka na matumbo yao moto.
HATULALI MPAKA KIELEWEKE!!!

No comments: