image slider

HUDUMA TUNAZOZITOA
Watengenezaji wa mashine za kuangulia vifaranga vya kuku
Wauzaji wa vifaranga vya kuku
Ushauri wa ufugaji wa kuku
Mashine za kuangulia vifaranga vya kuku
Wauzaji wa vifaranga vya kuku
Mashine za kuangulia vifaranga vya kuku

Saturday, August 3, 2013

Hatua za Tahadhari za Kuzuia Kuingia na Kuenea kwa Magonjwa Shambani


1. Tenganisha ndege kufuatana na aina ya ndege na umri wao
2. Weka karantini kwa ndege/kuku wapya ili wachunguzwe kwa kipindi kisichopungua wiki mbili
kabla ya kuingizwa shambani au bandani.
3. Usiruhusu tabia ya kuchangia vifaa/vyombo kama vile makasha ya mayai, makreti ya kubebea kuku
kati ya shamba na shamba, n.k.
4. Wafanyakazi waanze kuwahudumia kuku wenye umri mdogo kabla ya wale wenye umri mkubwa.
5. Usiruhusu watoto kucheza na kuku.
6. Jaribu kuzuia idadi ya wageni wanaoingia shambani/bandani.
7. Weka utaratibu wa kuangamiza mizoga ya kuku.
8. Anzisha programu jumuishi ya kudhibiti wadudu/wanyama waharibifu.
9. Panga utaratibu mzuri wa kuwapa kuku huduma ya maji na kufanya usafi.
10. Panga utaratibu mzuri wa kuzoa taka na mizoga ya kuku.
11. Panga utaratibu mzuri wa kusafisha banda na kupulizia dawa.
12. Vifaa visafishwe na kuwekwa dawa ya kuua vijidudu kabla ya kuingizwa shambani.
13. Hakikisha magari yanapoingia shambani yanapita katika kidimbwi chenye dawa ya kuua vimelea
vya magonjwa.
14. Hakikisha mfanyakazi anabadilisha viatu/mabuti kabla ya kuingia katika kila banda
15. Weka taratibu nzuri za kuingia shambani, ikiwa ni pamoja na kuhakikisha usafi wa viatu na mikono;
au wageni na wafanyakazi kubadilisha nguo/viatu na kuvaa mabuti.

No comments: