image slider

HUDUMA TUNAZOZITOA
Watengenezaji wa mashine za kuangulia vifaranga vya kuku
Wauzaji wa vifaranga vya kuku
Ushauri wa ufugaji wa kuku
Mashine za kuangulia vifaranga vya kuku
Wauzaji wa vifaranga vya kuku
Mashine za kuangulia vifaranga vya kuku

Friday, March 29, 2013

Sifa, Faida na Changamoto za Ufugaji wa Kuku wa Asili




Kuku wa Asili ni wale ambao wamekuwepo hapa nchini kwa miaka mingi na damu yao
haijachanganyika na ya kuku wa kigeni. Kuku hawa wana rangi na maumbo mbali mbali.
Idadi ya kuku wa Asili hapa Tanzania inakadiriwa kufikia milioni 56. Kati ya kaya milioni 3.8
zinazojishughulisha na kilimo nchini, kaya milioni 2.3 hujishughulisha na ufugaji wa kuku wa asili.
Kwa kawaida ufugaji wa kuku wa Asili hapa nchini kwetu Tanzania hufanywa na wafugaji wadogo
wadogo wanaoishi kando kando ya miji na wale wanaoishi vijijini. Kuku hawa hufugwa huria (freerange),
yaani hufungiwa ndani nyakati za usiku na hufunguliwa asubuhi ili wajitafutie chakula.
Kuku hawa hutoa mazao machache sana yaani nyama na mayai, kwa mfano kuku mmoja hutaga
kiasi cha mayai 40-60 kwa mwaka badala ya 100-150 iwapo atatunzwa vizuri. Pia uzito wa kuku
hai ni wa chini sana, wastani wa kilo 1.0–1.5 katika umri wa zaidi ya miezi 6 badala ya kilo 1.8–2.5
iwapo atatunzwa vizuri.
Sifa za Kuku wa Asili:
Wastahimilivu wa magonjwa, lakini ni muhimu wakikingwa na baadhi ya magonjwa ya kuku
kama mdondo, ndui ya kuku nk. ili kuweza kuwaendeleza.
Wana uwezo wa kujitafutia chakula ardhini, lakini ili kuwaendeleza ni lazima kuwapa chakula
bora cha ziada.
Wana uwezo wa kuatamia mayai, kutotoa, kulea vifaranga na ustahimilivu wa mazingira
magumu (ukame, baridi nk).
Nyama na mayai yake vina ladha nzuri kuliko kuku wa kisasa.
Kwa kiasi fulani wana uwezo wa kujilinda na maadui kama vile mwewe.
Pamoja na sifa hizi ni muhimu kuku hao wakapewa matunzo mazuri, wawekwe kwenye mabanda
mazuri na imara, pia wapewe maji na chakula cha kutosha.Faida za Ufugaji wa Kuku wa Asili:
Chakula – nyama ya kuku na mayai hutumika kama chakula muhimu cha wanadamu, chenye
protini.
Chanzo cha kipato – mkulima hupata fedha akiuza kuku au mayai.
Chanzo cha ajira – ufugaji wa kuku hutoa ajira kwa jamii.
Kuku hutumika kwenye shughuli za ndoa kama vile kutoa mahari na pia ni kitoweo muhimu
katika sherehe hizo.
Gharama nafuu za kuanzisha na kuendesha mradi huu.
Ni kitoweo rahisi na chepesi kwa wageni kuliko wanyama wakubwa kama ng’ombe au mbuzi.
Ni kitoweo kisichohitaji hifadhi, hutumika mlo mmoja au miwili na kumalizika.
Kuku na mayai hutumika kwa tiba za asili.
Jogoo hutumika kama saa anapowika nyakati za alfajiri na majira mengine ya siku.
Hutuhabarisha iwapo kiumbe kigeni au cha hatari kwa mlio maalum wa kuashiria hatari.
Mbolea – kinyesi cha kuku kinaweza kutumika katika kurutubisha mashamba ya mazao na
mabwawa ya samaki.
Kuendeleza kizazi cha kuku wa asili hapa nchini.
Soko lipo la uhakika, ukilinganisha na kuku wa kisasa kwani nyama na mayai yake hupendwa
zaidi na walaji.
Manyoya ya kuku hutumika kama mapambo, pia huweza kutumiaka kutengenezea mito ya
kulalia na kukalia.
Shughuli za utafiti – kuku wanatumika katika tafiti nyingi za baiolojia, kama kutambua mambo ya
lishe.
Shughuli za viwandani:
Mayai yenye mbegu ya jogoo hutumika katika kutengeneza dawa za chanjo.
Magamba ya mayai yanaweza kutumika katika utengenezaji wa vyakula vya wanyama.
Kiini cha njano cha mayai kinaweza kutumika kutengeneza mafuta ya kuoshea nywele
(shampoo).
Mapungufu ya Kuku wa Asili:
Hutaga mayai madogo wastani wa gramu 47 ambapo kuku wa kisasa wastani wa gramu 55,
aidha hutaga mayai machache wastani wa mayai 60 kwa mwaka ambapo kuku wa kisasa
huweza kutaga hadi mayai 300 kwa mwaka.
Ukuaji taratibu – kuku wa asili hukua taratibu kutokana na lishe duni. Kutokana na hali hiyo kuku
huchukua muda mrefu (miezi sita) kufikia uzito wa kuchinjwa (kilo 1 - 1.5). Hali hii pia hufanya
faida ya ufugaji wa kuku wa asili kuchukua muda mrefu kupatikana.
Nyama yake ni ngumu (huchukua muda mrefu kuiva) ikilinganishwa na kuku wa kisasa.
a.
b.
c.
d.
e.
f.
g.
h.
i.
j.
k.
l.
m.
n.
o.
p.



a.
b.
c.
Changamoto katika ufugaji kuku wa asili:
Mabanda: Ukosefu wa mabanda bora.
Wezi, wanyama na ndege hushambulia kuku.
Magonjwa: kama mdondo na ndui huathiri ufugaji wa kuku.
Tabia na miiko ya baadhi ya jamii. Baadhi ya jamii za makabila hapa nchini huona ufugaji wa
kuku kama ni kitu duni.
Upatikanaji haba wa chanjo za magonjwa kama vile, mdondo, ndui, homa ya matumbo.


No comments: