image slider

HUDUMA TUNAZOZITOA
Watengenezaji wa mashine za kuangulia vifaranga vya kuku
Wauzaji wa vifaranga vya kuku
Ushauri wa ufugaji wa kuku
Mashine za kuangulia vifaranga vya kuku
Wauzaji wa vifaranga vya kuku
Mashine za kuangulia vifaranga vya kuku

Tuesday, June 20, 2017

Mashine ya mayai 300

Hii mashine inabeba mayai 300 ni sh. 1700000. Inaenda kwa mteja wetu Mwanza. Ukihitaji incubator tupigie 0753903809
Mashine zetu zina ufanisi mkubwa sana.
Mashine hii ni "fully automatic".
Ndugu mjasiriamali, karibu sana!

Monday, June 19, 2017

Wednesday, June 7, 2017

Sunday, December 25, 2016

MASHINE ZA KUTOTOA VIFARANGA

Tupo mwishoni kabisa mwa mwaka
Katika kusaidiana kuondokana na umaskini, sisi tunafanya kila kinachowezekana kusaidiana katika jitihada za kupambana na umaskini.
Kwa sasa tuna mashine za kutotoa vifaranga zinazotumia mafuta ya taa na ufanisiwake ni zuri sana.
Kubwa kabisa ya hizi mashine za mafuta ya taa zinazotumia mafuta ya taa ni ile inayobeba mayai 120. Hii inapatikana kwa sh. 70000 tu.Bei za mashine zingine zimepungua bei kama ifuatavvyo:
MNAKARIBISHWA WOTE
MAWASILIANO NI: 0753903809 . Mashine za mafuta za mafuta ya taa ni nzuri kwa watu wanao ishi sehemu ambazo hazina umeme

Tuesday, October 25, 2016

Bei na aina mpya za mashine za kuangulia vifaranga vya kuku na ndege

1. Incubator ya mayai 120 sh. 1000000
2. Incubator ya mayai 180 sh 1200000
3. Incubator ya mayai 240 sh 1500000
4. Incubator ya mayai 300 sh. 1700000
5. Incubator ya mayai 360 sh. 1800000
6. Incubator ya mayai 420 sh. 2000000
7. Incubator ya mayai 600 sh. 2300000
8. Incubator ya mayai 1000 sh 2600000
10. Incubator ya mayai 1500 sh. 3600000
 KARIBUNI WOTE. BEI ZIMEPUNGUZWA
MASINE ZETU ZINA UWEZO MKUBWA SANA WA KUTOTOA KWA UFANISI MKUBWA SANA

Sunday, May 22, 2016

Bei mpya za mashine za kutotoa vifaranga toka tarehe 22/05/2016
Mashine ya mayai 180 = Tsh. 1500000 kama ya awali
Mashine ya mayai 300 = Tsh. 2000000 badala ya Tsh. 2200000 ya awali
Mashine ya mayai 600 = Tsh. 2500000 badala ya Tsh. 2800000 ya awali
Mashine ya mayai 1000 = Tsh. 3000000 badala ya Tsh. 3500000 ya awali
Mashine ya mayai 1500 = Tsh. 4000000
Mashine ya mayai 2000 = Tsh. 4500000
Mashine ya mayai 3000 = Tsh. 5000000

Karibuni sana wajasiriamali wote mnaopenda kujiinua kiuchumi kupitia ufugaji wa kuku wa kienyeji

Wednesday, January 13, 2016

UFUGAJI WA KUKU

UFUGAJI BORA WA KUKU WA KIENYEJI

Idadi ya wanyama wanaofugwa kwa chakula imezidi ile ya binadamu zaidi ya mara mbili kote ulimwenguni. Kuna maelfu ya wanyama kote duniani ilihali ni wachache tu wanaoweza kufugwa. Kati ya hawa wanyama, ni aina nne (Ng'ombe, kondoo, mbuzi na kuku) wanaochukua asilimia 95% ya wanyama wote wanaofugwa. Wanyama hawa hupatikana katika nchi za hari kwenye nyanda za chini. Lakini kati ya mifugo hawa, kuku ni maarufu katika nchi za hari na hata kote ulimwenguni.
Lengo la makala haya ni kutoa maelezo ili kusaidia wafugaji wa kiwango kidogo katika nchi
zinazostawi, katika kupunguza umaskini. Sehemu ya kwanza (I) itatoa maelezo kuhusu ufugaji na
hasa ufugaji wa kuku, Sehemu ya pili (II) itaangazia maswala yafuatayo katika kuinua hali ya uchumi
kwa kufuga kuku:
1. Kuendeleza ufugaji wa kuku za kienyeji kwa kutumia njia zisizohitaji gharama nyingi.
2. Kutafuta mbinu na njia muafaka za kuzalisha viwango vya kuku bora kwa njia ya kiasili.
3. Matumizi ya njia za kiasili au zile zisizo gharimu pesa nyingi kutibu na kuzuia magonjwa ya
kuku.

SEHEMU YA I: MAELEZO KUHUSU UFUGAJI WA KUKU KATIKA NCHI. ZINAZOENDELEA

NAFASI YA MIFUGO

Licha ya kukosa mashamba makubwa ya kuendeleza ufugaji wa ng'ombe, jamii nyingi katika nchi za
hari (tropics) hupata nafasi ya kufuga kuku kwa kiwango kidogo. Idadi ya wanyama wanaofugwa
huongezeka sambamba na ile ya watu. Idadi ya watu inapoongezeka ndipo ile ya mifugo huzidi.
Idadi kubwa ya watu huhitaji chakula kingi na matumizi huongezeka, hivyo basi watu hufanya bidii
kuzalisha chakula na mapato kutoka kwa shamba.
Ufugaji wa ng'ombe na wanyama wanaohitaji lishe kwa wingi huhitaji kiasi kikubwa cha shamba ili
kupanda mimea na lishe la mifugo. Ukilinganisha na ufugaji wa kuku, utahitaji mabaki ya vyakula
na sehemu ndogo ya shamba. Ufugaji wa kuku umeweza kunawiri hata pasipo fedha.
Katika nchi za hari ufugaji wa kienyeji hautahitaji kazi nyingi, kazi hii hufanywa na akina mama na
watoto. Kwa kawaida katika nchi hizi kazi nyingi za nyumbani hutekelezwa na mama. Vyakula vya
kuku vyaweza kutoka kwa: 1) Mabaki ya chakula, 2) Mabaki ya mimea, 3) Mabaki kutoka jikoni
na 4) Vyakula vya kujitafutia (kwa mfano kwekwe, mbegu, wadudu, nyongonyongo, n.k). Mfumo
wa kufuga kuku kwa njia ya kienyeji hutumia viungo vinavyopatikana kwa urahisi na kuimarisha hali
ya kiuchumi na chakula bora kwa jamii.
Ni muhimu sana kufuga mifugo hata ikiwa ni kwa kiwango kidogo kwa sababu ya 1) Chakula bora
na kuongeza mapato ya jamii kwa viwango vya kuridhisha; 2) Mifugo ni hakiba au banki, faida yake
huzaana tu kama riba ya benki; 3) Mifugo yaweza kuuzwa ili kugharamia karo ya wanafunzi,
malipo ya hospitali, gharama nyingine za nyumbani na hata shambani; 4) Kwa matumizi ya kijamii
(kwa mfano kulipia mahari, shughuli za kidini, n.k); 5) Mifugo husaidia katika kukabili wadudu,
kwekwe na kuimarisha rutuba kutokana na mbolea ya kinyesi. Ni bayana kwamba mifugo ni
muhimu sana kwa mkulima yeyote yule

UMUHIMU WA UFUGAJI WA NJIA YA KIENYEJI

Ufugaji wa kuku katika nchi zinazostawi waweza kugawanywa mara mbili: 1) Ufugaji wa
kitamaduni au kienyeji pasipo kuwepo gharama, na 2) Ufugaji wa kisasa unaohitaji fedha nyingi.
Ufugaji wa viwango vikubwa kwa kuzingatia mfumo wa kisasa ni maarufu katika kuzalisha kuku wa
nyama na wale wa mayai. Mfumo huu hujumuisha asilimia ndogo sana ya aina ya ufugaji.
Itafahamika kwamba mfumo wa kisasa haujaadhiri ule wa kienyeji. Idadi kubwa ya watu katika nchi
za hari hutegemea mfumo wa kienyeji kwa nyama na mayai.
Mfumo wa kisasa huhitaji pesa nyingi za kununua vyakula vya kuku. Aidha mfumo wa kisasa huhitaji kazi nyingi ili kutekeleza. Mfumo wa kisasa
umefaulu katika nchi zilizostawi kutokana na hali nzuri ya kiuchumi katika kuzalisha (kuku wa hali
ya juu, kuangua vifaranga kwa stima, vyakula vilivyo na madini mengi, vifaa na zana za mashine,
utaalamu wa hali ya juu n.k). Haitafaa sana kuanzisha mfumo kama huu katika vijiji vya mataifa
yanayostawi.
"Mageuzi" katika ufugaji (kuambatanisha mfumo wa kisasa pamoja na ule wa kienyeji) yamefanyiwa
majaribio katika mataifa yanayostawi tangu miaka ya 1950. Matokeo ya kuku wapatao 200 hadi 300
kwa shamba moja hayajawai kufaulu. Hasara imepatikana na waweza kuona nyumba zilizokuwa na
kuku bila chochote, pesa nyingi zimepotea na kuku hawapo.
Mfumo wa kienyeji ni bora (Katika hali ya kiuchumi) iwapo idadi ya kuku haitazidi kuku 50. Ni
rahisi kuweza kuwatunza kuku, kwani hakuna gharama nyingi. Iwapo vyakula au zana za kisasa
zitanunuliwa, basi haitakuwa kwa viwango vikubwa. Mazao ya nyama na mayai yataleta faida.
Sehemu nyingi katika mataifa yanayostawi hakuna stima, katika nchi za hari, ufugaji kwa kiwango
kidogo umeweza kufaulu na kuimarisha uchumi.

FAIDA ZA UFUGAJI WA KUKU KWA NJIA YA KIENYEJI

Faida za uzalishaji kuku ili kuimarisha uchumi kwa njia hii zimepuuzwa na viongozi na wafadhili.
Kuku huleta faida kwa jamii kama tulivyoona katika sehemu ya I. Zaidi ya hayo, ufugaji wa kuku waweza kuimarishwa pasipo gharama nyingi ukilinganisha na mifugo wengine.
· Hutupatia fedha kwa kuuza nyama na mayai
· Mayai ni chakula kilicho na madini muhimu na kisicho ghali katika soko lolote. (madini kama methionine na cystine), madini haya ni muhimu sana kwa afya ya watu hasa watoto wachanga. Pia hutupatia protini.
· Kinyesi cha kuku ni mbolea safi
· Kiwanda asilia cha kutotoa vifaranga
· Gharama za kuanzisha na kuendeleza ni nyepesi
· Kitoweo chepesi na rahisi kwa wageni, kitoweo hakihitaji hifadhi hutumika mlo mmoja au miwili na kumalizika
· Jogoo hutumika kama saa inapowika
· Manyoya ya kuku hutumika kutengenezwa mapambo mbalimbali, mito na magodoro
· Kuku wanahisimu wadudu waharibifu
Kuku ndiye mnyama wa kipekee anayeweza kuishi mahali popote hapa ulimwenguni bila kuadhiriwa
na viwango vya hali ya hewa. Ufugaji wa kuku ndio shughuli inayofanyika kwa wingi duniani kuliko ufugaji wa aina yeyote. Kuku hunawiri vyema katika nchi za hari kutokana na uwiano uliopatikana wakati wa mwanzo binadamu alipofuga Asian jungle fowl aina ya kuku-mwitu. Mayai pia yaweza kuhifadhiwa kwa urahisi na huchukua nafasi ndogo kuliko aina ya bidhaa zozote za mifugo. Mayai yaweza kuwekwa mahali kwa muda mrefu bila kuhitaji barafu. Hautahitaji kuhifadhi kuku kwa njia yoyote, kwani nyama yake hupatikana pale unapohitaji kwa kuchinja.

Upungufu wa kuku wa kigeni ukilinganisha na wale wa kienyeji ni kama ufuatao:

• Kuku wa kigeni hawawezi kukalia na kuangua mayai, hivyo basi wahitajika kununua vifaranga (gharama);
• Vifaranga wa kigeni huhitaji utunzaji maalum na vyakula maalum (gharama);
• Kuku waliozalishwa kwa njia ya kisasa huhitaji chakula kingi ili kutaga mayai (gharama);
• Kuku wa kisasa huhitaji zaidi kuchanjwa dhidi ya magonjwa (gharama)ukilinganisha na wa kienyeji (japo nao huhitaji chanjo);
• Kuku wa kutaga mayai huhitaji mwangaza wa stima (saa 14 kwa siku) ili kutaga mayai (gharama)
Kwa kuongezea, rangi ya nyama na mayai ya kuku wa kienyeji huvutia kuliko ile ya kuku wa kisasa.
Hivyo basi jaribu kuendeleza na kuhimiza ufugaji wa kuku za kienyeji.
Iwapo mkulima ana jogoo mmoja na kuku kumi na mbili, basi kila mwezi waweza kupata kuku
akikalia mayai 10-12 kwa mwezi (mayai yote kwa wakati mwingi hayataanguliwa) kuna hakikisho la
kupata vifaranga vinne kila mwezi. Kuku mzima atachukua miezi minne kuchunga vifaranga
walioanguliwa. Kwa hivyo, kati ya kuku wote kumi na mbili kila mara kutakuwa na kuku wanne
wakitunza vifaranga, huku wale wengine wanane wakitaga mayai.
Kuku waliofugwa kwa njia ya kitamaduni hupata vyakula vyao kwa kutafuta mbegu, wadudu
nyongonyongo, n.k; Lakini kuku hawa hukosa vyakula vya kutosha vilivyo na nguvu ili waweze
kutaga mayai. Vyakula vya kutoa nguvu daima huwa ni haba.
Waweza kuwalisha kuku kwa nafaka ili wapate chakula cha nguvu (mfano kilo moja ya nafaka
iliyopondwa kila siku kwa kuku 10), nafaka hii yapaswa kuwa kavu. Vifaranga wapewe kiasi kidogo
cha nafaka au mchele wiki za kwanza. Kuku wanaolishwa nafaka baada ya kujitafutia chakula nje
huongeza idadi ya mayai (kutoka asilimia 20-25% hadi 40-50%). Kuna umuhimu wa kuhifadhi
nafaka kama lishe badala ya kuuza kwani utapata mayai mengi ambayo baadaye utaweza kuuza.
Hautahitaji kununua vyakula vya protini kwani kuku hujitafutia lishe la protini.
Ikiwa hauna nafaka, waweza kutumia vyakula vya mzizi au ndizi. Vyakula vya aina hii hata hivyo,
huwatatiza kuku wanapovitonogoa, kiwango cha mayai sio kikubwa kama cha wale wanaolishwa
nafaka.
Kwa kuwalisha kuku kwa nafaka utapata hakikisho la mayai manne kwa siku kutoka kwa wale kuku
wanane. Iwapo hakuna nafaka, kati ya kuku wanane wanaotaga utapata mayai mawili tu kwa siku.
Ni bora kutumia nafaka hii kama lishe kuliko kuuza na hatimaye kununua vyakula vya dukani.
Kuku kumi na mbili na jogoo mmoja wanaolishwa kwa kilo moja ya nafaka kila siku waweza
kuelezwa hivi:
• Waweza kuuza kuku wanne kila mwezi na kujaza pengo hilo na wale vifaranga (vifaranga
wanne huanguliwa kila mwezi) na
• Dazani kumi za mayai kila mwezi (mayai manne kila siku).
Kwa mwaka mmoja waweza kukadiri ile faida utakayopata na vile hali ya kiuchumi yaweza
kuinuliwa katika mataifa yanayostawi.
Hata hivyo faida hii haitaafikiwa iwapo magonjwa
hayatazuiwa au kukabiliwa kama ifuatavyo.

TEKELEZA UTARATIBU WA KUZUIA MAGONJWA

Magonjwa ndio husababisha hasara katika mfumo wa ufugaji wa kuku. Kuku waliochanjwa dhidi ya
magonjwa hudumisha afya bora. Jaribu kila mara kuzuia magonjwa, kwani kuzuia ni bora kuliko
kuponya. Kinga yaweza kutolewa mara kwa mara (kila baada ya miezi mitatu) dhidi ya magonjwa
yafuatayo:

Ugonjwa wa Newcastle

Ugonjwa huu ndio huadhiri kuku na kusababisha hasara katika nchi za hari. Virusi vya ugonjwa huu
huenea kwa kasi na rahisi kiasi cha kusababisha vifo kwa asilimia 100%. Dalili za kwanza ni shida
ya kupumua na kung'amua hewa, sauti kama ya kikohozi na kutokwa mate. Kinyesi chaweza kuwa
na rangi ya kijani kibichi. Hadi sasa hakuna dawa.
Waweza kuzuia ugonjwa huu kwa kutoa chanjo. Dawa za chanjo hupatikana kote ulimwenguni hata
katika nchi za hari kwenye vipimo vya vitone mia moja. Madawa haya yaweza kuhifadhiwa kwa
muda. Waweza kuweka kwa wiki moja mbali na jua au joto kali (Chanjo hii ni ya kipekee, kwani
aina nyingine ya chanjo huwekwa kwa friji). Waweza kutoa chanjo kwa kutia vitone kwenye
mdomo. Kuku wote (wakubwa kwa wadogo) wapaswa kupewa chanjo baada ya kila miezi mitatu.

Minyoo

Minyoo kama chango (roundworms) na tegu (tapeworms) huadhiri kuku wa kienyeji. Kuku hukosa hamu ya chakula, mayai hupungua na magonjwa mengine hushambulia. Ni bora basi kutoa minyoo.
Mchanganyiko wa madawa ya aina tatu ndio hutumiwa kuangamiza minyoo, madawa haya ni
piperazine, phenothiazine na butynorate. Madawa haya hupatikana kama vidonge (tumia kidonge 1
kwa kuku mzima na 1/2 kwa vifaranga). Iwapo hautapata dawa hii, waweza kutumia Panacur au
dawa nyingine ya kuangamiza minyoo. Wapatie kuku dawa ya minyoo kila baada ya miezi mitatu.

Wadudu

Wadudu kama chawa au utitiri husumbua kuku katika ufugaji wa kienyeji. Chawa au utitiri
husababisha harara ya ngozi, kuku walio adhiriwa hupata shida na kukosa usingizi. Hali hii
hupunguza kiwango cha mayai na uzito wa kuku.
Tumia asilimia 5% ya unga wa malathion kwa kupulizia kuku (puliza kwa chupa uliyo toboa
mashimo) pulizia kila kuku ili kuzuia chawa na utitiri (kilo moja ya unga huu yaweza kutibu kuku
150). Pulizia dawa hii baada ya kila miezi mitatu, waweza kupuliza kwa wakati mmoja wa kutoa
chanjo na dawa zilizotajwa hapo juu. Puliza unga huu pia kwenye viota vya kuangulia mayai.
Waweza kutayarisha 5% ya malathion kwa kuchanganya 25% ya unga wa malathion (kiwango cha
kilimo) na sehemu nne za jivu kutoka jikoni.

Magonjwa ya mapafu

Magonjwa ya mapafu huadhiri njia inayopitisha hewa na kuambatanisha mate na sauti kama ya
kikohozi. Ugonjwa huu huenea polepole. Uambukizanaji pia hutokea kwa polepole na vifo sio kwa
wingi. Hata hivyo, kutaga mayai na uzito hupungua. Shida hii yaweza kusambaa hata kutoka mahali vifaranga huanguliwa hadi pale walipouzwa.
Tylosin19 ndio dawa inayoweza kutibu magonjwa ya mapafu. Kiasi cha 35mg ya tylosin hutosha
kuku mmoja (kiwango hiki hufaa kuku na hata vifaranga) dawa hii husimamisha madhara kutokana
na magonjwa ya mapafu. Tibu kuku kila baada ya miezi mitatu, waweza kutekeleza kwa wakati
mmoja wa kutoa kinga na kuangamiza minyoo. Tylosin hupatikana kwa pakiti ndogo ya 4gm.
Waweza kutayarisha dawa hii kwa kutumia maji na 35gm ya tylosin (gramu nne kwa vikombe viwili
vya maji), kiasi hiki chaweza kutolewa kwa vitone kwa kila kuku

KWA UFUPI (SUMMARY)

Kabila za Kuku

Si rahisi kupata kabila halisi (pure breed) au kizazi halisi (pure line) za kuku wa kienyeji kutokana na mwingiliano wa vizazi kati ya aina mbalimbali za kuku hao. Lakini hata hivyo baadhi ya kuku wa kienyeji wanaweza kutambuliwa kutokana na maumbile yao kwa mfano

1. Kuchi

Warefuna wenye kusimama mgongo ukiwa wima
Wana manyoya machache mwilini na vilemba vyao ni vidogo
Majogoo huwa na wastani wa kilo 2.5 na mitetea kilo 1.8
Mayai gram 45

2. Ching'wekwe (Umbo dogo)

Hupatikana zaidi Morogoro na umasaini
Majogoo kilo 1.6
Mitetea kilo 1.2
Yai gram 37
kuku hawa wanafaa sana kwa biashara ya mayai kwa kuwa hutaga mayai mengi sana.

3. Umbo la Kati

Majogoo kilo 1.9
Mitetea kilo 1.1
Mayai gramu 43
Hukua upesi na hupata kinga upesi baada ya kuwachanja dhidi ya ugonjwa wa Mdondo (New Castle)

4. Singamagazi

Hupatikana zaidi Tabora
Majogoo wana rangi ya moto na mitetea rangi ya nyuki
Majogoo kilo 2.9
Mitetea kilo 2
Mayai gramu 56

5. Mbeya

Wanapatikana Ileje Mbeya na asili yao ni Malawi
Mjogoo kilo 3
Mitetea kilo 2
Mayai gramu 49
Uwezo wao wa kuatamia mayai na kuangua ni mdogo sana ukilinganisha na kuku wengine

6. Pemba

Maumbo ya wastani na miili myembamba
majogoo kilo 1.5
mitetea kilo 1
mayai gramu 42

7. Unguja

Hawatofautiani sana na wa Pemba
Vilemba vyake ni mchanganyiko- vidogo an vikubwa
Majogoo kilo 1.6
Mitetea kilo 1.2
Mayai gramu 42


Monday, December 7, 2015

VIFARANGA VIFARANGA VIFARANGA

Tunawakaribisha wateja wetu wote kujipatia vifaranga vya bata mzinga. Mjini Iringa
Namba zetu ni 0753903809

Wednesday, July 1, 2015

UFUGAJI WA KUKU KWA FAIDA NA TIJA

Wajasiriamali wengi hupenda miradi ambayo huwaletea matokeo au faida mapema,
Mradi wa kufuga kuku ni mradi ambao huleta faida kwa muda mfupi sana.
Ili upate faida kubwa ni vizuri ukawa na mradi ambao unaweza kuumudu kwa kuwa na mahitaji muhimu katika mradi wako.
MFANO, mtu anayetaka kufuga kuku tuseme 500 anatakiwa kuwa na vifaranga 550. Awe ana uwezo wa kuwalisha hao vifaranga na kuwapa tiba. Pia awe na uwezo wa kujenga banda bora.

 Baada ya hapo kinachotakiwa ni umakini wa kufuatilia mradi katika kipengele cha utoaji huduma kwa kuku hao. Katika kundi hilo la kuku 500, 50 wanatakiwa kuwa majogoo na 450 mitetea.
Katika hao mitetea 450 aslimia 75 wanatakiwa watage kila siku. Asilimia 75 ya 450 ni kuku 337. 
Mayai ya kuku hawa huuzwa kwa Tsh. 300@. Hivyo kila siku utapata Tsh 337 x 300 = Tsh. 100000.
Kama mtu anaweza kupata Tsh. 100000 kila siku kwa mwezi una uhakika angalau wa kuweka akiba ya Tsh. 100000 bila shida. Kama utaweka akiba ya fedha hiyo kila mwezi bila shida kwa mwaka utakuwa umeweka akiba ya shilingi milioni kumi na mbili.
Watu wengi wanaweza kufikiri hii ni nadharia ambayo haiwezekani, UKweli ni kuwa hiki kitu kinawezekana bila shida kabisa.
Ikiwa utahitahiji usaidizi njoo kwetu tukuelekeze namna unavyoweza kuondokana na umaskini usio wa lazima.
Kumbukeni ndugu wajasiriamali kwamba ukiamua ni kweli ndoto yako itatimia.
KARIBUNI SANA 0753903809
Kwetu tunafanya haya:
1. Tunauza mashine za kutotoa vifaranga
2. Tunauza vifaranga
3. Tunatoa ushauri

Saturday, January 3, 2015

Mwaka 2015 kwa nguvu mpya na maarifa mapya

Napenda kuwapa heri ya mwaka mpya wajasiriamali wote. Nategemea mwaka huu wajasiriamali wengi zaidi wataungana nasi katika kujikwamua na umaskini huu.
Nawashauri ndugu zanguni kufanya kazi halali kwa bidii kuliko kukaa ukiota eti kuna siku utaingiziwa fedha za ESCROW na fulani.
Kwa wale wanaotaka kuondokana na umasikini kwa njia ya ufugaji wa ndege mbalimbali kama kuku na kware tuwasiliane kwa namba hapo juu.
Mashine zetu za kuangulia vifaranga zinaendelea kutengenezwa kwa bei zifatatazo
- Incubator ya mayai 180 = Tsh 1,500,000
- Incubator ya mayai 300 = Tsh 2,200,000
- Incubator ya mayai 600 = Tsh 2,800,000
- Incubator ya mayai 1000 = Tsh 3,500,000
KARIBUNI WOTE

Saturday, June 28, 2014

HABARI NJEMA KWA WAFUGAJI WA KUKU NA NDEGE WA AINA ZOTE

Ndugu wapendwa wajasiriamali wenzangu, napenda kuwashirikisha jambo hili muhimu ambalo tukilizingatia kwa akili zetu zote na nguvu zetu zote huku tukimshirikisha Muumba wetu atujalie afya tele tunaweza kuondokana na madhila haya ya umaskini.
FikiriMungu amekujalia tabia ya ujasiriamali na wewe ukachagua kufuga kuku tuseme kuku wa kienyeji.
Katika harakati zako ukabahatika kununua mashine ya kuangua vifaranga (incubator). Tuseme mashine hiyo inabeba mayai elfu moja na ni nzuri imetoka kwa fundi aliyebobea maana kwa busara kabla ya kununua imefanya utafiti uone nani fundi kweli na mashine zake zina ufanisi mkubwa.
Baada ya kupata mashine umenunua mayai ya Tsh. 350000. Unaweka kwenye mashine yako unapata labda tuseme vifaranga 850. Kuangalia unakuta mashine yako imetumia umeme wa Tsh 50000. Umetafuta wateja wa vifaranga wako ukapata na vyote vikachukuliwa kwa kila kimoja Tsh. 2000 maana katika eneo lako hiyo ndo bei. Kihesabu hapo utakuwa umetapata Tsh. 1700000. Ukitoa Tsh 350000 uliyonunulia mayai na Tsh. 50000 ya umeme unabaki na kiasi gani ndugu mjasiriamali? Mimi situmii calculator hapa ila natumia uzoefu wa kitu ambacho nimekifanya kabisa na kwangu Tsh. 1400000 inabaki mfukoni kama faida.
Sasa ndugu mjasiriamali unangoja nini? Njoo tuongee kwa pamoja tuondokane na unyonge huu kwa kufanya kazi halali ambayo haina manung'uniko yoyote.
USHAURI NI KUWA USIJARIBU KUNUNUA MASHINE ZA KUANGUA VIFARANGA KABLA HUJAFANYA UTAFITI UKAONA UFANISI WA HIZO MASHINE.
HABARI NJEMA KWA WAJASIRIAMALI
Kwa sasa tunatengeneza mashine za kuangua vifaranga zaukubwa mbalimbali kama ifuatavyo:
1. Mashine za mayai 90 = Tsh. 600,000/
2. Mashine za mayai 120 = Tsh 800,000/
3. Mashine za mayai 180 =Tsh. 1,500,000/
4. Mashine za mayai 300 =Tsh. 2,200,000/
5. Mashine za mayai 600 =Tsh. 2,800,000/
6. Mashine za mayai 1000 = Tsh. 3,500,000/
 Mashine zetu zina sifa nzuri sana za uanguaji mzuri wa mayai. Mnakaribishwa wote mfike mjionee zinavyofanya kazi. Sisi tupo Iringa mjini. Mnakaribishwa sana.


Monday, December 9, 2013

BEI MPYA ZA MASHINE ZA KUANGUA VIFARANGA

HABARI NJEMA KWA WAJASIRIAMALI
Kwa sasa tunatengeneza mashine za kuangua vifaranga zaukubwa mbalimbali kama ifuatavyo:
1. Mashine za mayai 90 = Tsh. 600,000/
2. Mashine za mayai 120 = Tsh 800,000/
3. Mashine za mayai 180 =Tsh. 1,500,000/
4. Mashine za mayai 300 =Tsh. 2,200,000/
5. Mashine za mayai 600 =Tsh. 2,800,000/
6. Mashine za mayai 1000 = Tsh. 3,500,000/
 Mashine zetu zina sifa nzuri sana za uanguaji mzuri wa mayai. Mnakaribishwa wote mfike mjionee zinavyofanya kazi. Sisi tupo Iringa mjini. Mnakaribishwa sana.








Thursday, September 19, 2013

Tuesday, September 17, 2013

BEI YA MASHINE ZA KUANGUA VIFARANGA

Tunazo mashine za kuangua vifaranga za ukubwa mbalimbali kama ifuatavyo:
1. Mashine ya mayai 180 = Tsh. 1,500,000
2. Mashine ya mayai 300 =Tsh. 2,200,000
3. Mashine ya mayai 600 =Tsh 2,700,000
4. Mashine ya mayai 1000 = Tsh3,5000,000
5. Mashine ya mayai 1500 = Tsh. 4,300,000
KUMBUKA 
Mashine zetu zina sifa zifuatazo:
1. Joto lake huoneshwa kwa kidhibiti joto cha kidijitali
2. Mashine zetu hugeuza mayai zenyewe (automatic incubators)
3. Mashine zetu hazina usumbufu kabisa na spea zake ni nyepesi kupatikana
4. Mashine zetu zina ufanisi wa hadi aslimia tisini (90% efficiency)
5. Mashine zetu haziharibiki mara kwa mara
KARIBUNI WOTE
Sisi tupo Iringa mjini. Watu wengi wamedai mashine zao zina ufanisi mkubwa tofauti na ukweli. Ukitaka kununua mashine kwetu tunakushauri ututembelee kwanza ili uonane na watengenezaji lakini pia uonane na wale ambao wanazitumia ili wakupe ushahidi wa jinsi mashine hizi zinavyoweza kutotoa vifaranga kwa ufanisi mkubwa bila usumbufu.
Kwa mawasiliano:
0753903809 au 0655903809
Mnakaribishwa sana

Saturday, August 10, 2013

Tofauti za muonekano kati ya kuku mwenye afya na kuku mgonjwa

Kuku mwenye afya nzuri
Macho na sura angavu
Hupenda kula na kunywa maji
Pua zilizo safi, upanga na undu mwekundu, manyoya
laini na yaliyopangika vizuri
Hupumua kwa utulivu
Sehemu ya kutolea haja huwa kavu
Kinyesi kikavu, cheupe na kisicho na rangi
Hutaga mayai kawaida
Kuku asiye na afya nzuri (mgonjwa)
Huonekana mchovu na dhaifu
Hula na kunywa kidogo au zaidi ya kawaida
Hutoa kamasi puani, ute na matongotongo; manyoya
yaliyovurugika
Hupumua kwa shida na kwa sauti
Sehemu ya kutolea haja inakuwa na unyevunyevu na
kinyesi kuganda
Huharisha, kinyesi huwa na damu au minyoo
Hutaga mayai machache au husimama kutaga kabisa
Huwa na tabia ya kujitenga na wenzake katika kundi

Mdondo/Kideri (Newcastle Disease)
Maelezo
Ni ugonjwa unaosababishwa na virusi ambao hushambulia aina zote za spishi za ndege, ijapokuwa kuku ndio aina
inayoathirika zaidi. Binadamu na wanyama wengine pia wanaweza kuambukizwa. Ugonjwa huathiri mifumo ya
fahamu, njia ya chakula na hewa.
Jinsi Ugonjwa Unavyoenea
• Chanzo cha maambukizi ni maji, chakula kilichochafuliwa na kinyesi cha kuku wagonjwa. Pia maambukuzi
huweza kupitia mfumo wa hewa kutoka kwa kuku wagonjwa.
• Kuku, vifaa vya kazi na bidhaa zitokanazo na kuku (nyama, mayai, manyoya na mbolea) kutoka mashamba
yenye ugonjwa zinaweza kueneza ugonjwa kutoka shamba moja hadi jingine.
• Vifaranga wanaweza kupata maambukizi kutoka vituo vya kutotolea vifaranga kutokana na maganda ya
mayai yaliyochafuliwa.
Dalili
• Vifo vya ghafla vya idadi kubwa ya kuku katika shamba/banda
• Kuku wanatetemeka na kushindwa kutembea
• Kuku hupooza miguu, mabawa na kupinda shingo; na hujizungusha mahali alipo
• Kuku huharisha kinyesi cha kijani na wakati mwingine chenye mchanganyiko wa rangi ya njano
• Kuku huzubaa na kuacha kula
• Kuku hukohoa, hupiga chafya na kupumua kwa shida
• Vifo vinaweza kufikia asilimia 100, kutegemea na umri na aina ya ndege
Uchunguzi wa Mzoga
Ugonjwa huathiri zaidi mfumo wa hewa na njia ya chakula, hivyo mabadiliko yanayoonekana kwenye mzoga ni
pamoja na:
• Madoa ya damu kwenye mfumo wa hewa
• Kamasi nzito zenye rangi ya njano kwenye koromeo
• Utandu mweupe kwenye mifuko ya hewa
• Bandama kuvimba
• Uvimbe kwenye kichwa na eneo la shingo
• Madoa madogo madogo ya damu kwenye kifua, mafuta na utandu wa tumboni
• Damu kuvia kwenye mfumo wa usagaji chakula - juju, firigisi, tumbo na utumbo
Tiba
• Hakuna tiba ya ugonjwa huu ila kuku wapewe antibiotiki.
• Pata ushauri wa daktari.
Kuzuia na Kinga
• Weka utaratibu wa kuhakikisha wafanyakazi , wageni na ndege hawaingii hovyo kwenye shamba/banda
• Angamiza mizoga yote kwa njia stahiki kwa kuchoma moto au kufukia kwenye shimo refu ardhini.
• Hakikisha banda la kuku lina hewa ya kutosha na epuka msongamano mkubwa wa kuku.
• Fanya usafi wa mara kwa mara kwenye vyombo vya kuwekea maji na chakula, pamoja na mabanda ya
kuku.
• Zuia uingizaji holela wa kuku wageni wasiochanjwa kwenye shamba/banda. Kuku wanaoingia shambani/
bandani watoke maeneo yasiyokuwa na ugonjwa.
• Tenganisha kuku kufuatana na umri
• Maeneo yenye ugonjwa yawekwe chini ya karantini na mabanda yapulizwe dawa
• Kuku wapewe Chanjo tangu vifaranga wa umri wa siku 3, baada ya wiki 3 – 4, na baadaye kila baada ya
miezi 3.

Saturday, August 3, 2013

Hatua za Tahadhari za Kuzuia Kuingia na Kuenea kwa Magonjwa Shambani


1. Tenganisha ndege kufuatana na aina ya ndege na umri wao
2. Weka karantini kwa ndege/kuku wapya ili wachunguzwe kwa kipindi kisichopungua wiki mbili
kabla ya kuingizwa shambani au bandani.
3. Usiruhusu tabia ya kuchangia vifaa/vyombo kama vile makasha ya mayai, makreti ya kubebea kuku
kati ya shamba na shamba, n.k.
4. Wafanyakazi waanze kuwahudumia kuku wenye umri mdogo kabla ya wale wenye umri mkubwa.
5. Usiruhusu watoto kucheza na kuku.
6. Jaribu kuzuia idadi ya wageni wanaoingia shambani/bandani.
7. Weka utaratibu wa kuangamiza mizoga ya kuku.
8. Anzisha programu jumuishi ya kudhibiti wadudu/wanyama waharibifu.
9. Panga utaratibu mzuri wa kuwapa kuku huduma ya maji na kufanya usafi.
10. Panga utaratibu mzuri wa kuzoa taka na mizoga ya kuku.
11. Panga utaratibu mzuri wa kusafisha banda na kupulizia dawa.
12. Vifaa visafishwe na kuwekwa dawa ya kuua vijidudu kabla ya kuingizwa shambani.
13. Hakikisha magari yanapoingia shambani yanapita katika kidimbwi chenye dawa ya kuua vimelea
vya magonjwa.
14. Hakikisha mfanyakazi anabadilisha viatu/mabuti kabla ya kuingia katika kila banda
15. Weka taratibu nzuri za kuingia shambani, ikiwa ni pamoja na kuhakikisha usafi wa viatu na mikono;
au wageni na wafanyakazi kubadilisha nguo/viatu na kuvaa mabuti.

Wednesday, June 26, 2013

KARIBUNI TUSHIRIKIANE KUUONDA UMASKINI KWA KUBUNI MIRADI ISIYOHITAJI MITAJI MIKUBWA

MRADI WA KUFUGA KUKU WA KIENYEJI
Katika maisha kila mtu hutamani sana kufikia mafanikio makubwa kwa kadri anavyoweza.
Kutamani kufikia mafanikio ni hulka ya mwanadamu. Sisi Watanzania tunazo fursa nyingi sana ambazo tukizichangamkia tunaweza kufanikiwa sana na kujivunia Utanzania wetu.
Pamoja na kuwa na fursa za kujiajiri, Watanzania wengi hawana wazo la kujiajiri kama walivyo majirani zetu kama Kenya.
Kwetu sisi Watanzania uwanja ya ajira binafsi ni bado ngeni sana. Bado namba ya watu kwa mfano wanaomaliza chuo na kuwa na wazo la kujiajiri ni ndogo sana hapa Tanzania.
Hii inatokana na mfumo wa elimu tunayopata hapa kwetu. Elimu tunayoipata haimuandai mtu kuwa mbunifu vya kutosha na kuwenza kuwa na mawazo ya kuchagua ajira binafsi dhidi ya ile ya kufanya kazi serikalini au mashirika ya watu wengine.
Muda umefika kwetu sisi watanzania wa kuchagua ajira binafsi. Tukiingia huko faida ni kubwa sana maana uzalishaji utaongezeka.
Mimi binafsi nimeamua kujikita kwenye biashara ya kufuga kuku baada ya kuacha kazi serikalini. Nimeacha kazi baada ya kuona sipati muda wa kufanya kile ambacho nafikiri kingeweza kuniondoa kwenye dimbwi la umaskini. Huko nilikofanyia kazi nilikutana na watu wapo kazini zaidi ya miaka 30 lakini hawakukoma kulalamika kwamba kazi wanayofanya haikuwafikisha pale walipotegemea kufika walipoanza kazi. Nilipoona hata mimi naanza kulalamika nikaondoka haraka sana maana nilijishtukia kwamba si muda mrefu ningeungana na walalamikaji.
MJIUNGE NAMI TUFUGE
Kwa wale wanaotaka kufuga, mnaweza kununua mashine za kuangulia vifaranga kutoka kwetu na tunawenza kuwasiliana kwa namba 0753903809 au 0655903809.
Mashine zenu ni nzuri na zenye ufanisi mkubwa sana na zina guarantee. Mashine zetu ni automatic kwa maana kuwa zinasoma joto kwa digital display na hizi display ni very sensitive to temperature changes.
Mashine zetu zinageuza mayai zenyewe. Zinageuza mayai kila saa kwa maana kuwa zinageuza mayai mara 24 kwa siku na hivyo kuongeza utotolekaji wa mayai. Effficiency (ufanisi) yake ni mpaka 90% na hii ina ushahidi maana tunakuruhusu kuwatembelea wafugaji ambao tayari wana mashine zilizonunuliwa kwetu.
KARIBUNI SANA. SISI TUNAPATIKA IRINGA MANISPAA