image slider

HUDUMA TUNAZOZITOA
Watengenezaji wa mashine za kuangulia vifaranga vya kuku
Wauzaji wa vifaranga vya kuku
Ushauri wa ufugaji wa kuku
Mashine za kuangulia vifaranga vya kuku
Wauzaji wa vifaranga vya kuku
Mashine za kuangulia vifaranga vya kuku

Saturday, January 1, 2011

KATIBA MPYA HIYOOOOOO!!!

Ndugu Watanzania wenzangu wapendwa, duniani hapa tupo ili kuhakikisha maisha yanaendelea bila matatizo yoyote.
Shida zinazojitokeza na kutufanya tuishi kwa shida zimeletwa na sisi wenyewe.
Ili kuhakikisha kila mmoja wetu anashiriki kupanga namna vile angependa kuishi kwenye nchi hii aliyopewa na Mwumba wake, ni vema kila mmoja wetu ashiriki kikamilifu kutoa maoni kuhusu katiba mpya ya nchi yetu.
Kwa Tanganyika, huu ndo mwaka pekee ambao tunapata wasaa wa kuirudisha nchi yetu Tanganyika na tukizubaa tu basi katiba itakayokuja itatufanya tuishi kwa kugugumia kwa miaka mingine hamsini.
Mimi napendelea kati ya haya:
1: Tuwe na serikali moja ya Tanzania
2: Kama 1 ni ngumu, basi tuwe na serikali tatu, yaani serikali ya Tanganyika, serikali ya Zanzibar na serikali ya Muungano.

0753903809